Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema, NCCR-Mageuzi wapigwa ‘stop’ Tarime
Habari za SiasaTangulizi

Chadema, NCCR-Mageuzi wapigwa ‘stop’ Tarime

Spread the love

MSIMAMIZI Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata ya Turwa wilayani Tarime, Mara amesitisha mikutano yote ya kampeni ya vyama vya upinzani kwenye kata hiyo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa hizo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii kupitia barua inayodaiwa kutolewa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Turwa, Peter Julius yenye kichwa cha habari; KUSITISHWA KWA KAMPENI ZA UCHAGUZI KWA CHAMA CHA NCCR-MAGEUZI KUANZIA TAREHE 10/08/2018 HADI 11/08/2018’.

Sehemu ya barua hiyo inaeleza kuwa, hatua hiyo imekuja baada ya NCCR-Mageuzi kudaiwa kukiuka sheria ya taifa ya uchaguzi.

“Nakujulisha kwa kufuatia chama tajwa hapo juu kukiuka kifungu cha 124A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343, Maadili ya Uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani ya mwaka 2015, Kamati ya Maadili ya Uchaguzi Kata ya Turwa kupitia kikao kilichoketi tarehe 10/08/2018 kimesitisha kampeni za chama hicho kwa muda wa siku mbili kuanzia tarehe 10/08/2018 hadi 11/08/2018,” inaeleza sehemu ya barua hiyo.

Kabla ya NCCR-Mageuzi kusitishwa kufanya kampeni kata ya Turwa, Chadema pia ilisitishwa kufanya kampeni za udiwani kwenye kata hiyo.

Barua hiyo imeeleza kwamba, kuanzia leo kampeni zitaendelea kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) pekee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!