MSIMAMIZI Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata ya Turwa wilayani Tarime, Mara amesitisha mikutano yote ya kampeni ya vyama vya upinzani kwenye kata hiyo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Taarifa hizo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii kupitia barua inayodaiwa kutolewa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Turwa, Peter Julius yenye kichwa cha habari; KUSITISHWA KWA KAMPENI ZA UCHAGUZI KWA CHAMA CHA NCCR-MAGEUZI KUANZIA TAREHE 10/08/2018 HADI 11/08/2018’.
Sehemu ya barua hiyo inaeleza kuwa, hatua hiyo imekuja baada ya NCCR-Mageuzi kudaiwa kukiuka sheria ya taifa ya uchaguzi.
“Nakujulisha kwa kufuatia chama tajwa hapo juu kukiuka kifungu cha 124A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343, Maadili ya Uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani ya mwaka 2015, Kamati ya Maadili ya Uchaguzi Kata ya Turwa kupitia kikao kilichoketi tarehe 10/08/2018 kimesitisha kampeni za chama hicho kwa muda wa siku mbili kuanzia tarehe 10/08/2018 hadi 11/08/2018,” inaeleza sehemu ya barua hiyo.
Kabla ya NCCR-Mageuzi kusitishwa kufanya kampeni kata ya Turwa, Chadema pia ilisitishwa kufanya kampeni za udiwani kwenye kata hiyo.
Barua hiyo imeeleza kwamba, kuanzia leo kampeni zitaendelea kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) pekee.
Leave a comment