HAKIMU mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba ametoa siku saba kwa upande wa Jamhuri kubadilisha hati ya mashtaka ili kuwaondoa kwenye kesi aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe na Frank Lauwo kwenye kesi ya utakatishaji fedha inayowakabili Evans Aveva na Godfrey Nyange (Kaburu). Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Hakimu huyo amesema kuwa washtakiwa hao wanatakiwa kuondolewa kwenye kesi hiyo kutokana na kutohudhulia mahakamani hapo hata siku moja hivyo kufanya shauri hilo kuchelewa kusikilizwa na itafika mahali uvumilivu utawashinda na kama Jamhuri wameshindwa bora waifute.
Kwa upande wa wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai ameieleza mahakama hiyo kuwa, kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na tayari wameshaifanyia marekebisho hati ya mashtaka na kwamba wanasubiri kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ili kesi hiyo iendelee na kesi hiyo imeahilishwa hadi 17 agosti mwaka huu.
Leave a comment