Wednesday , 27 September 2023
Home Kitengo Michezo Hans Poppe kuondolewa kwenye kesi ya Aveva, Kaburu
Michezo

Hans Poppe kuondolewa kwenye kesi ya Aveva, Kaburu

Spread the love

HAKIMU mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba ametoa siku saba kwa upande wa Jamhuri kubadilisha hati ya mashtaka ili kuwaondoa kwenye kesi aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe na Frank Lauwo kwenye kesi ya utakatishaji fedha inayowakabili Evans Aveva na Godfrey Nyange (Kaburu). Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Hakimu huyo amesema kuwa washtakiwa hao wanatakiwa kuondolewa kwenye kesi hiyo kutokana na kutohudhulia mahakamani hapo hata siku moja hivyo kufanya shauri hilo kuchelewa kusikilizwa na itafika mahali uvumilivu utawashinda na kama Jamhuri wameshindwa bora waifute.

Kwa upande wa wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai ameieleza mahakama hiyo kuwa, kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na tayari wameshaifanyia marekebisho hati ya mashtaka na kwamba wanasubiri kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ili kesi hiyo iendelee na kesi hiyo imeahilishwa hadi 17 agosti mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

BiasharaMichezo

Piga pesa kupitia Derby ya London Kaskazini kwa kubadhiri na Meridianbet

Spread the love NAJUA umesikia na unazijua Derby nyingi kutoka jiji la London,...

error: Content is protected !!