Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge laanza, Waziri Mkuu kuulizwa maswali 16  
Habari za Siasa

Bunge laanza, Waziri Mkuu kuulizwa maswali 16  

Spread the love

MKUTANO wa 12 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unatarajiwa kuanza Jumanne ya tarehe 4 Septemba 2018, huku maswali 16 ya papo kwa papo yakimsubiri Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa siku ya Alhamisi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).  

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 3 Septemba 2018 kwa vyombo vya habari na Kitengo cha Habari, Elimu kwa Umma na Mwasiliano Ofisi ya Bunge, inaeleza kuwa, Katika Mkutano huo wa 12, wastani wa maswali 125 ya kawaida yanatarajiwa kuulizwa na Wabunge.

Katika mkutano huo, kutakuwa na kiapo cha uaminifu kwa Eng. Christopher Kajoro Chizza, Mbunge wa Jimbo la Buyungu aliyechaguliwa kwenye Uchaguzi Mdogo tarehe 12 Agosti, 2018.

Pia Bunge linatarajia kupitisha kwa hatua zilizobaki miswada mitano ya sheria iliyosomwa mara ya kwanza katika mkutano wa 11 wa bunge ikiwemo muswada wa kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya nchi wa mwaka 2018 na muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi wa mwaka 2018.

katika mkutano huo, Kamati ya Sheria Ndogo itawasilisha taarifa zake Bungeni zinazohusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa na Bunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!