MKUTANO wa 12 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unatarajiwa kuanza Jumanne ya tarehe 4 Septemba 2018, huku maswali 16 ya papo kwa papo yakimsubiri Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa siku ya Alhamisi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Taarifa iliyotolewa leo tarehe 3 Septemba 2018 kwa vyombo vya habari na Kitengo cha Habari, Elimu kwa Umma na Mwasiliano Ofisi ya Bunge, inaeleza kuwa, Katika Mkutano huo wa 12, wastani wa maswali 125 ya kawaida yanatarajiwa kuulizwa na Wabunge.
Katika mkutano huo, kutakuwa na kiapo cha uaminifu kwa Eng. Christopher Kajoro Chizza, Mbunge wa Jimbo la Buyungu aliyechaguliwa kwenye Uchaguzi Mdogo tarehe 12 Agosti, 2018.
Pia Bunge linatarajia kupitisha kwa hatua zilizobaki miswada mitano ya sheria iliyosomwa mara ya kwanza katika mkutano wa 11 wa bunge ikiwemo muswada wa kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya nchi wa mwaka 2018 na muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi wa mwaka 2018.
katika mkutano huo, Kamati ya Sheria Ndogo itawasilisha taarifa zake Bungeni zinazohusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa na Bunge.
Leave a comment