Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko ‘Boda to boda’ kuzinduliwa kesho
Habari Mchanganyiko

‘Boda to boda’ kuzinduliwa kesho

Dk. Augustine Mahinga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Spread the love

SHIRIKA lisilo la kiserikali la Foundation For Civil Society (FSC) kesho linatarajia kuzindua kampeni ya “Chungulia Fursa Boda to Bado,” anaandika Victoria Chance.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, Boniphace Makene, Afisa Mawasiliano wa shirika hilo, amesema “ lengo la kampeni hii ni kuwahamasisha vijana na wanawake kuzitambua fursa za kibiashara na uchumi zilizopo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.”

“Kampeni zitazinduliwa na Balozi Dk. Augustine Mahinga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na tunatarajia kupata washiriki kutoka taasisi 150 ambazo tunafadhili shughuli zao,” amesema Makene.

Makene amesema mbali na kampeni hizo kuzinduliwa jijini Dar es Salaam pia zitaendeshwa katika majiji ya Arusha na Mwanza kwa kuwa ndiyo maeneo makuu ya kibiashara.

“Mafunzo yatakayotolewa kupitia kampeni hii wafanyabiashara wadogo wataongezewa kujiamini na kuwafungua macho kwenye fursa mbalimbali za biashara zinazofanywa katika mipaka ya nchi yetu,” amesema Makene.

Katika kampeni hiyo wamewaalika wafanyabiashara wakubwa kwa lengo la kuwapa changamoto wafanyabiashara wadogo kwa kuwaelezea njia walizopitia mpaka kufikia mafanikio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!