Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bashange ataka ukatibu mkuu ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Bashange ataka ukatibu mkuu ACT-Wazalendo

Spread the love

JORAM Bashange, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi na Kampeni ya Chama cha ACT-Wazalendo, amechukua fomu ya kugombea nafasi ya katibu mkuu kwenye chama hicho. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Leo tarehe 10 Februari 2020, Bashange amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo kwenye Makao Makuu ya chama hicho, Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.

Baada ya kuchukua fomu hiyo, Bashange amesema kuwa amejipima na kufanya tafakuri binafsi, na kuona anatosha kwenye nafasi hiyo.

“Nimesoma Katiba na kuona majukumu yake, nimeangalia kanuni za kudumu za uendeshaji wa chama na kufanya tafakuri binafsi na kuona, kwamba nafasi hii inanitosha kuitumikia,” amesema.

Uchukuaji fomu za kugombea nafasi mbalimbali za chama hicho, ulianza tarehe 27 Januari 2020, na utakamilika tarehe 26 Februari 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!