Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko BAKWATA yampinga “Mtume wa uongo” Pwani
Habari Mchanganyiko

BAKWATA yampinga “Mtume wa uongo” Pwani

Msemaji Mkuu wa Mufti, Khamis Mataka
Spread the love

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limewataka waumini wake na watanzania wote nchini kumpuuza mtu mmoja aliyejitokeza huko mkoani Pwani, akidai kuwa yeye ni Nabii Ilyasa, anaandika Irene David.

Mwenyekiti wa Halmashauri BAKWATA taifa na Msemaji Mkuu wa Mufti, Khamis Mataka, amethibitisha kuwepo na upotoshwaji wa mafundisho ya Uislamu yatolewayo na Hamza Issa, “Mtume Ilyasa” wakati akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya baraza hilo jijini Dar es Salaam.

Issa anadai kuwa yeye ni Muislam amepewa ufunuo na kwamba roho ya ”Mtume Ilyasa” imemuingia na hivyo yeye ndiye “Nabii Ilyasa” mwenyewe.

Anatumia Qurani na mafunzo ya kiislamu jambo lililosababisha Baraza la Masheihk wa mkoa wa Pwani kutolifumbia macho na kuleta maazimio yao kwa Mufti Mkuu.

Kwa mujibu wa Imani yetu sisi Waislam, tunaamini kuwa hakuna Nabii aliyekuwepo na atakaye kuja kuwepo tena zaidi ya Nabii na Mtume Mohammad.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!