Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Awamu ya Tano: Watumishi 32,555 ‘waisoma namba’
Habari za Siasa

Awamu ya Tano: Watumishi 32,555 ‘waisoma namba’

Seleman Jafo
Spread the love

JUMLA ya watumishi 32,555 wamechukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu ikiwemo kufukuzwa kazi, kushushwa vyeo na kushushwa mishahara katika serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Waliokutwa na dhoruba hizo ni wale waliobainika kuwa wazembe kazini, kughushi vyeti, rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Kauli hiyo imetolewa na Rais John Magufuli leo Jumanne tarehe 16 Juni 2020, bungeni jijini Dodoma, katika hafla ya ufungaji wa shughuli za Bunge la 11.

“Kama tulivyoahidi, hatutakuwa na mzaha kwa viongozi na watumishi wazembe walioshindwa kufanya kazi kwa weledi, nidhamu, maalifa na uadilifu. Waliobainika walichukuliwa hatua za kinidhamu ikiwemo kuwatumbua, kuwashusha vyeo na mishahara au kuwapa onyo kali,” amesema Rais Magufuli.

Rais wa Tanzania, John Magufuli

Kiongozi huyo wa Tanzania amesema, katika uongozi wake, watumishi 15,508 waliachishwa kazi baada ya kukutwa na vyeti vya kughushi, alifuta ajira hewa 19,708 zilizokuwa zikigharimu Sh. 19.8 bilioni na kwamba, hatua hiyo ilitoa fursa ya kaujiri watumishi wapya 74,173.

Pia amesema, serikali yake imefanikiwa kuwapandisha vyeo watumishi 306,967 na kulipa madeni mbalimbali ya watumishi kiasi cha Sh. 472.6 Bil., ambapo ya kimshahara ni Sh. 114.5 Bil., na yasiyo ya kimshahara Sh. 358.1 Bil.

Serikali ya Rais Magufuli alianza kuongoza Tanzania Novemba 2015. Serikali imetambulika zaidi kwa mtindo wa ‘kutumbua’ watumishi walioonekana kutokwenda sawia na mwendo wa serikali hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!