Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yabariki CCM kumsulubu Zitto
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yabariki CCM kumsulubu Zitto

Spread the love

WAKATI Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakipanga kumsulibu Zitto Kabwe, Chama cha ACT Wazalendo kimebariki mkakati huo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

ACT-Wazalendo kimeshauri Wabunge wa CCM kujipanga kwa hoja kwa kuwa, hoja za Zitto, Kiongozi Mkuu wa chama hicho na Mbunge wa Kigoma Mjini ni zenye kutafitiwa.

Ado shaibu, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa ACT Wazalendo ametoa taarifa ya msimamo wa chama hicho na kusambazwa na Zitto mwenyewe.

Taarifa hiyo inatokana na dhamira ya wabunge CCM kutaka kumkabili Zitto kwa madai ya kumsumbua Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri pia upotoshaji.

Baada ya kukutana kwenye Kamati ya Wabunge wa CCM (Caucus) wamemwona mbunge huyo ni adui namba moja.

Ado na ACT-Wazalendo wanaungana na dhamira ya CCM dhidi ya Zitto ila kwa kupambana kwa hoja.

Amesema, walichopanga kukifanya wabunge wa CCM, bila kujali wanatumia hoja yenye uzito gani kujibu, ndiyo maana hasa ya siasa.

“Kutarajia mashambulizi ya hoja za kisiasa kujibiwa kwa vitisho na mabavu ya vyombo vya dola kama ambavyo imeanza kujengeka katika miaka ya hivi karibuni ni utamaduni wa ovyo.” Amesema na kuongeza;

“Kumtisha, kumdhuru au kumuweka korokoroni mtoa hoja badala ya kuikabili hoja yake si siasa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!