Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo waitetea kauli ya Halima Mdee
Habari za SiasaTangulizi

ACT-Wazalendo waitetea kauli ya Halima Mdee

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT
Spread the love

NGOME ya Vijana ya chama cha ACT-Wazalendo, imesema kuna hatari ya utawala wa sheria nchini kuporomoka endapo watanzania hawatapigania sheria na amani ya nchi, anaandika Hamisi Mguta.

Hayo yameelezwa leo na Karama Kaila, Mwenezi wa Ngome ya Vijana ya chama hicho, katika tamko lao ikiwa ni siku nne tangu kukamatwa kwa Halima Mdee, Mbunge wa Kawe (Chadema) kwa amri ya Ally Hapi, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni (DC).

“Tukumbuke kuwa wazee wetu waliopigania uhuru wa nchi hii hawakufanya hivyo kumuondoa mtu mwenye ngozi nyeupe, bali walifanya hivyo wakitarajia kuondoa kila aina ya uonevu dhidi yao ikiwemo kubanwa kwa uhuru wa kujieleza na kujiamulia mambo yao bila kuvunja sheria,” amesema Kaila.

Karama Kaila, Mwenezi wa Ngome ya Vijana ya chama cha ACT-Wazalendo

DC Hapi aliagiza Mdee akamatwe na kuwekwa ndani kwa saa 48 Julai 4 kwa kudai kuwa alitoa maneno ya kukashifu na ya uchochezi katika mkutano wake wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) uliofanyika Julai 3 makao makuu ya chama hicho alipozungumza kuhusu msimamo wao kwa wanafunzi waliopata mimba kurudi shuleni.

Kaila amesema baadhi ya wateule wa rais wamegeuza kauli mbalimbali kutoka kwa rais kama sehemu ya kuwakomoa wenye mawazo tofauti na kauli au matakwa ya rais, huku akisisitiza kuwa misingi ya utawala bora ni kuheshimu katiba ya nchi ambayo ndiyo sheria mama.

“Amri ya mkuu wa wilaya ya kinondoni kuamuru kukamatwa na kuwekwa kizuizini kwa mbunge wa Kawe ni matumizi mabaya ya sheria na uvunjifu wa katiba ya nchi ambayo viongozi wa umma wameapa kuilinda na kuisimamia.

“Tunasema hivi kwa sababu Mdee hakumtukana rais wala hajatoa maneno yoyote yenye viashiria vya uvunjifu wa amani kama anavyodai DC Alli Hapi,” amesema Kaila.

1 Comment

  • Hata katiba imesema; hakuna uhuru usiokuwa na kikomo. Hata maandiko yamesema “kuweni na kiasi”!
    Jitafakarini!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!