Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto amkumbuka Maalim Seif
Habari za SiasaTangulizi

Zitto amkumbuka Maalim Seif

Spread the love

 

KIONGOZI wa Chama Cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema chama chake kinaendelea kumuenzi aliyekuwa Mwenyekiti wake Taifa, Maalim Seif Shariff Hamad, aliyefariki Dunia tarehe 17 Februari 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akitoa ujumbe wake wa kumbukumbu ya miaka miwili ya kifo Cha Maalim Seif, leo tarehe 17 February 2023, kupitia ukurasa wake wa Twitter, Zitto amesema ACT-Wazalendo itaendeleza harakati zake kuimarisha demokrasia na kupigania muungano wa haki nchini.

“Tunakuenzi kwa kuendeleza harakati za kuimarisha demokrasia nchini na kupigania muungano wa haki, heshima na usawa. Tunaendelea kusimamia maridhiano ya Wazanzibari na kuongoza juhudi za maridhiano ya Watanzania. Tunakukumbuka kwa vitendo Maalim!,” ameandika Zitto.

Maalim Seif pamoja na wafuasi wake, walijiunga na ACT-Wazalendo 2019, kupitia opereshenj yake ya shusha tanga, pandisha tanga, wakitokea Chama cha Wananchi (CUF), baada ya kukosa muafaka katika mgogoro wa kiuongozi uliokuwa unakikabili chama hicho, baada ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kumtambua Prof. Ibrahim Lipumba, kuwa mwenyekiti halali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!