Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Z’bar ‘yawabana’ watalii kulinda utamaduni
Habari za Siasa

Z’bar ‘yawabana’ watalii kulinda utamaduni

Baadhi ya Watalii wakiwa kisiwani Zanzibar
Spread the love

 

SERIKIALI ya Mapinduzi Zanzibar imewataka watalii kuzingatia miiko na maadaili ya Mzanzibari hasa katika mavazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, imewataka wageni na watalii kuzingatia miongozo ya maadili ambayo imekuwa ikitolewa na taasisi zinazosimamia Utalii.

“Wizara inatoa tahadhari kwa wananchi wa Zanzibar, wadau wa utalii na wageni wanaotembeleza Zanzibar kuzingatia maadili na utamaduni wa Kizanzibari, ili kuiepusha na usumbufu wa adhabu za kisheria zitakazochukuliwa dhidi yao,” imeeleza taarifa hiyo.

Imefafanua, katika siku za karibuni kumekuwa na ukiukwaji wa mila, maadili na utamaduni wa Kizanzibari hasa katika suala la mavazi.

“Hali hii hujitokeza kwa baadhi ya wageni na watalii wanaotembelea Zanzibar kwa kushindwa kufuata maadili yanayotaka kuvaa nguo za stara, hasa wanapokuwa kwenye mijumuiko na maeneo mengine ya Umma,” imeeleza taarifa hiyo.

Wizara hiyo mesema jambo hilo si tu limekuwa kero, lakini pia ni kinyume cha sheria za nchi.

Imeeleza, serikali imeonesha kutopendezwa na hali hiyo, hivyo imewasiliana na ofisi za ubalozi za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika nchi mbalimbali duniani, na kuwapatia machapisho mbalimbali na video fupifupi kuhusu maadili ya utalii ya Zanzibar.

Imeeleza kwamba, lengo la kutoa machapisho hayo ni waziwasilishe kwenye taasisi za nchi wanazoziwakilisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!