Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yapitisha vigogo 5 baraza la wadhamini
Michezo

Yanga yapitisha vigogo 5 baraza la wadhamini

Mama Fatma Karume, Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Yanga
Spread the love

 

MKUTANO Mkutano Mkuu wa Klabu ya Yanga ya Dar es Salaam, imepitisha majina matano likiwemo Mama Fatuma Karume, kuwa wajumbe wa Baraza la Wadhamini wa timu hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Majina hayo, yamepitishwa leo Jumapili, tarehe 27 Juni 2021, katika mkutano mkuu huo wenye lengo la kufanya mabadiliko ya katiba ili kuifanya kuendeshwa kisasa.

Kabla ya kupitishwa, Mweneykiti wa Yanga, Dk. Mshindo Msolla ameyatangaza mbele ya wajumbe majina hayo likiwemo la Mama Fatma ambaye ni mjane wa Rais wa kwanza wa Zanzibar, Abeid Aman Karume.

George Mkuchika

Wengine ni; mawaziri wa serikali ya Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba wa Fedha na Mipango na Kepteni mstaafu George Mkuchika, Waziri Ofisi ya Rais-Kazi Maalum.

Pia, wamo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Uwekezaji, Geofrey Mwambe na Mbunge wa Kinondoni (CCM), Abbas Tarimba.

Abbas Tarimba

Wajumbe hao watano, watamchagua mwenyekiti pindi watakapokutana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!