Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wazungu wadaiwa kumteka kimafia MO Dewji
Habari Mchanganyiko

Wazungu wadaiwa kumteka kimafia MO Dewji

Mohamed Dewji 'MO Dewji'
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limeeleza kuwa, linawashilikia watu watatu wanaoshukiwa kuhusika na tukio la kutekwa kwa Mfanyabiashara Mohammed Dewji, lililotokea alfajiri ya leo tarehe 11 Oktoba 2018, katika Gym ya hoteli ya Colosseum iliyoko Oysterbay jijini Dar es salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, amewaambia wanahabari kuwa, MO Dewji anayedaiwa kutekwa kimafia, alitekwa na wazungu wawili waliokuwa na silaha za moto.

Kamanda Mambosasa ameeleza kuwa, wazungu hao wawili waliwasilia hotelini hapo wakiwa na gari binafsi aina ya Surf ambalo walilipaki karibu na gari ya MO Dewji, kisha kumchomo mfanyabiashara huyo ndani ya gari lake na kumpakia kwenye gari lao, na kuondoka naye kusikojulikana.

Kwa mujibu wa taarifa za awali zilizo tolewa na mashuhuda wa tukio hilo, inasemekana watu hao walikuwa wanne huku wakiwa wamefunika nyuso zao ‘Ninja’, walifyatua risasi hewani kuwatishia watu waliokuwa karibu na eneo hilo kabla ya kuondoka naye.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!