Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Wazungu wadaiwa kumteka kimafia MO Dewji
Habari Mchanganyiko

Wazungu wadaiwa kumteka kimafia MO Dewji

Mohamed Dewji 'MO Dewji'
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limeeleza kuwa, linawashilikia watu watatu wanaoshukiwa kuhusika na tukio la kutekwa kwa Mfanyabiashara Mohammed Dewji, lililotokea alfajiri ya leo tarehe 11 Oktoba 2018, katika Gym ya hoteli ya Colosseum iliyoko Oysterbay jijini Dar es salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, amewaambia wanahabari kuwa, MO Dewji anayedaiwa kutekwa kimafia, alitekwa na wazungu wawili waliokuwa na silaha za moto.

Kamanda Mambosasa ameeleza kuwa, wazungu hao wawili waliwasilia hotelini hapo wakiwa na gari binafsi aina ya Surf ambalo walilipaki karibu na gari ya MO Dewji, kisha kumchomo mfanyabiashara huyo ndani ya gari lake na kumpakia kwenye gari lao, na kuondoka naye kusikojulikana.

Kwa mujibu wa taarifa za awali zilizo tolewa na mashuhuda wa tukio hilo, inasemekana watu hao walikuwa wanne huku wakiwa wamefunika nyuso zao ‘Ninja’, walifyatua risasi hewani kuwatishia watu waliokuwa karibu na eneo hilo kabla ya kuondoka naye.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!