Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Mchengerwa atoa maagizo wanaoajiriwa serikali
Habari za Siasa

Waziri Mchengerwa atoa maagizo wanaoajiriwa serikali

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imewataka waajiri wote nchini humo katika taasisi za umma kuhakikisha watumishi wanaoajiriwa kwenye taasisi zao wanapata mafunzo elekezi kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kabla ya kuanza kazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Lengo ni kuhakikisha azma ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alitaka utumishi wa umma kuwa uliotukuka.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa jana Alhamisi, tarehe 18 Novemba 2021, wakati akizindua bodi ya ushauri ya chuo hicho.

Mchengerwa alisema, mafunzo watakayoyapata watumishi hao yatasaidia kuwajenga kimaadili, kutambua na kuiishi miiko ya utumishi wa umma, kujua mwelekeo wa Serikali, kuwa na mienendo sahihi inayotakiwa katika utumishi wa umma na kuwajengea uzalendo kwa taifa.

“Mafunzo haya ni muhimu sana kwa watumishi wa umma kuwajenga kiutendaji kwasababu leo hii ukipita kwenye taasisi za umma utabaini baadhi ya watumishi hawako hai kiutendaji kwa sababu ya kukosa mafunzo elekezi ambayo yangewajengea nidhamu ya utendaji kazi,’’ alisema Mchengerwa

Waziri huyo alisema, ukosefu wa mafunzo kwa watumishi wa umma yanasababisha baadhi ya watendaji na watumishi kutoelewana kwasababu binafsi hali inayofanya baadhi ya watendaji kutowapangia majukumu watumishi walio chini yao hivyo taifa linakosa mchango wao wakati Serikali inawalipa mshahara.

Katika kushughulikia masuala ya nidhamu ya watumishi wa umma, Mchengerwa aliwataka waajiri kuzingatia taratibu za kushughulikia masuala ya nidhamu ili kulinda haki za watumishi wa umma.

Awali, naibu waziri wa wizara hiyo, Deogratius Ndejembi ali sema Chuo cha Utumishi wa Umma kina jukumu kubwa la kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Umma na kuwaandaa wanaoingia kwenye Utumishi wa Umma ili wawe na mwenendo bora.

Alisema, chuo hicho hakitakiwi kushindana na vyuo vingine kwasababu hata wahiti

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!