Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Pablo wa Simba kibaruani leo
Michezo

Pablo wa Simba kibaruani leo

Spread the love

KOCHA mpya wa klabu ya Simba Pablo Franco Martin, leo kwa mara ya kwanza atakiongoza kikosi cha Simba kwenye kibarua chake cha kwanza, dhidi ya Ruvu Shooting kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Mchezo huo ambao utapigwa kwenye dimba la Ccm Kirumba, Mwanza ambao utakuwa wa kwanza kwa kocha huyo toka alipokuja kuchukua mikoba ya Didier Gomes Da Rossa.

Akizungumza na waandishi wa Habari jana jijini Mwanza, Pablo alisema kuwa, anategemea kuibuka na matokeo kwenye mchezo huo, licha ya kukili kuwa Ruvu Shooting ni moja ya timu ngumu na wanacheza vizuri.

“Tutagemea kesho kupata mechi ngumu, hio timu inacheza mchezo mzuri na mgumu na tuliona walivyocheza na Yanga ni aina ya timu nzuri.” Alisema kocha huyo

Pablo anaiongoza timu hiyo ambayo ipo kwenye presha kwa sasa kutokana na matokeo waliyoyapa hivi karibuni, licha ya usajili mkubwa walioufanya kwenye dirisha la usajili mara baada ya kumalizika kwa Ligi msimu uliopita.

Aidha kocha huyoa aliongezea kuwa, kikosi chake kipo tayari kwa mchezo huo na kupambania alama tatu ambazo zitawaweka vizuri kwenye mchezo wa Ligi.

 “Tupo tayari kwa ajili yamchezo wa kesho (leo) najua utakuwa mchezo mzuri  na tupo tayari kupambana na kupata pointi tatu.” Alisema kocha huyo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!