Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Waziri Aweso awafyeka vigogo wa maji
HabariTangulizi

Waziri Aweso awafyeka vigogo wa maji

Juma Aweso, Waziri wa Maji
Spread the love

 

WAZIRI wa Maji nchini Tanzania, Jumaa Aweso, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (Ruwasa), Mhandisi Deusdedith Magoma. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea)

Taarifa iliyotolewa na kitengo cha mawasiliano cha wizara hiyo jana Jumanne tarehe 16 Februari 2021, imesema, Waziri Aweso ameagiza Magoma kurejeshwa wizara ya maji “apangiwe majukumu mengine.”

Waziri Aweso, amemteua Mhandisi Ndele Mwansanga, kukaimu nafasi ya Magoma, wakati taratibu nyingine za kiutumishi za kumthibitisha kwenye nafasi hiyo zikiendelea.

Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi Mwansanga, alikuwa mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya majisafi na usafiri wa mazingira jijini Mbeya (Mbeya Uwasa).

Kutokana na uteuzi huo wa Mhandisi Mwansanga, Waziri Aweso amemhamisha kituo cha kazi mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Iringa (Iruwasa), Gilbert Kayange kwenda kuchukua nafasi ya Mhandisi Mwansanga jijini Mbeya.

Katika kupanga vyema safu ya sekta ya maji, Waziri Aweso, ameagiza Bodi ya Ruwasa kutengua uteuzi wa meneja wa ujenzi wa Ruwasa makao makuu pamoja na meneja wa Ruwasa Mkoa wa Geita na “wapangiwe kazi nyingine ndani ya Ruwasa.”

Pia, Waziri Aweso, ameagiza bodi hiyo, kutengua uteuzi wa mameneja wa Ruwasa katika wilaya 20 za; Buhingwe, Uvinza, Mbulu, Musoma, Mbarali, Rungwe, Tandahimba, Nkasi, Kishapu, Baruadi, Songwe, Uyui, Misungwi, Magu, Bukoba, Babati, Igunga, Bunda, Ikungi na Newala na kutaka nafasi hizo zijazwe ndani ya wiki moja kwa kuteua watumishi walioonyesha bidii za kiutendaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari

Serikali yataka vijana  wajiunge na program atamizi ya biashara CBE

Spread the love  SERIKALI imewahamasisha vijana kujiunga na program atamizi inayotolewa na...

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

error: Content is protected !!