Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Michezo Wateja wa betPawa wajishindia bilioni 53.8
Michezo

Wateja wa betPawa wajishindia bilioni 53.8

Spread the love

Wateja 333,706 wa kampuni ya Michezo ya kubashiri betPawa wameweka rekodi ya ushindi katika mchezo huo baada ya kujishindia Sh 53.8 bilioni ndani ya siku 10. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Wateja hao walisherehekea ushindi katika mchezo huo wa kubashiri kwa usahihi kwenye michezo kati ya Jumamosi tarehe 21 na Jumatatu tarehe 30 Oktoba mwaka huu.

Meneja wa betPawa nchini Borah Ndanyungu alisema mshindi wa kwanza aliyejinyakulia kitita kikubwa kuliko wote, alishindia Sh 372.9 milioni kwa dau la Sh2,200, ikiongezewa na bonasi ya ushindi ya asilimia 645 kwenye mechi 50 alizobashiri.

“Hii imedhihirisha kauli mbiu ya ‘betPawa pesa kidogo’, ushindi mkubwa (Bet Small, Win BIG) kwa jumla wateja 3,738 wa betPawa Tanzania walibadilishwa kuwa mamilionea kwa kipindi cha ndani ya siku 10.

“Kutokana na idadi hii kubwa ya washindi ambayo haijawahi kutokea ilisababisha ucheleweshaji wa malipo katika tasnia nzima ya michezo ya kubashiri. Kwetu betPawa kuwa na washindi wengi kumesababisha akaunti zetu za mitandao ya simu kulazimika kuongezwa kiwango cha pesa kila mara kulingana na kiwango cha juu kinachoruhusiwa kwa siku,” alisema na kuongeza kuwa;

“Hata hivyo tunafanya kazi saa 24 ili kumalizia malipo ya washindi wachache waliosalia.”

Aidha, Ndanyungu alisema hakuna mtu bora kuliko wateja wa betPawa ambao wamefanikiwa kupata ushindi mkubwa, na katika kipindi hiki cha siku 10 wameshinda zaidi kuliko hapo awali.

“Tunafahamu idadi kubwa ya ushindi umesababisha ucheleweshaji katika tasnia nzima ya michezo ya kubashiri na sisi betPawa tunafurahi kuwa tayari tumeweza kulipa washindi wengi tayari mpaka sasa. Tunafanya kazi bila kuchoka ili washindi wachache waliobakia mwisho walipwe,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Pesa ipo huku Meridianbet, beti sasa

Spread the love  WIKIENDI inaishia leo hii jaman kama bado hujasuka mkeka...

Michezo

Wenzako wameshakuwa mamilionea hapa wewe unasubiri nini?

Spread the love  WIKIENDI imefika na ukiachana na mvua za Dar es...

Michezo

Manchester City vichwa chini Ligi Kuu England

Spread the love MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Uingereza klabu yaManchester City...

Michezo

Piga mkwanja wa kutosha katika usiku wa kibabe kati ya Man United vs Chelsea

Spread the love USIKU wa leo katika dimba la Old Trafford utapigwa mchezowa...

error: Content is protected !!