Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Watakao kiuka taratibu uchaguzi CCM kufyekwa
Habari za Siasa

Watakao kiuka taratibu uchaguzi CCM kufyekwa

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo
Spread the love

 

KATIBU mkuu wa Chama cha Mapinduzi(CCM),Daniel Chongolo ametangaza kuwafyeka wagombea nafasi za uongozi ndani ya chama hicho endapo watakiuka misingi na utaratibu wa chama hususani kuanza kampeni mmapema na kujihusisha na vitendo vya rushwa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Chongolo ametoa taadhari hiyo leo Jumatano tarehe 13 Julai, 2022, akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wenyeviti wa ngazi ya matawi na mashina waliochaguliwa ndani ya chama hicho kwa Mkoa wa Dodoma.

Chongolo amesema kuwa wapo baadhi ya wanachama ambao kwa sasa wanaanza magenge ya kunyemelea nafasi mbalimbali zikiwemo za ubunge na nafasi nyingine ya juu jambo ambalo ni kinyume na utaratibu ndani ya chama.

“Ninataka kuwaambia wanachama wa chama cha Mapinduzi kuwa nitawachukulia hatua kali wanachama wote ambao wanaendeleza makundi ndani ya chama chetu na wengine upitapita kutafuta nafazi ndani ya chama.

“Lazima mkajua kuwa kwa sasa tunatambua kuwa viongozi waliopo ndiyo wanaotambulika lakini hatuna mbunge mwingine, diwani wala Rais tunajua muda wa kuanza kampeini bado.

“Mtu yoyote ambaye anatengeneza makundi kwa ajili ya kumchafua mtu mwingine kwakudhani anatengeneza njia ya kupata nafasi fulani tutamshughulikia kisawasawa na kwa bahati mbaya tunawajua na wanachokifanya tunakijua.

” Hatutasita kuwachukulia hatua kali hata kuwafuta uanachama kwani hatuna hasara nao wala faida nao. Kwa mtu wa aina hiyo hatavumiliwa na atachukuliwa hatua kwani chama chetu hakitaki makundi ya kuchafuana badala yake kinatakiwa kufanya kazi kwa kufuata misingi, taratibu, sheria na kanuni,” ameeleza Chongolo.

Katika hatua nyingine Chongolo ameweka jiwe la misingi katika jengo la kitega uchumi cha CCM lenye vyumba 172 ambapo hadi unakamilika mradi huo utagharimu kiasi cha Sh920 milioni na kuingiza Sh1.8 bilioni kwa mwaka baada ya kukamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!