Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Watafiti wa mbegu watakiwa kufuata kanuni
Habari Mchanganyiko

Watafiti wa mbegu watakiwa kufuata kanuni

Mbegu za mahindi
Spread the love

WATAFITI wa mbegu ndani na nje ya nchi wametakiwa kufuata sheria na kanuni zilizowekwa na Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) katika kutafiti mbegu mpya na kusajiliwa kwa wakati ili ziwafikie mapema wakulima katika msimu husika, anaandika Christina Haule.

Mkurugenzi Mkuu wa TOSCI, Patrick Ngwediagi amesema taasisi yake inavyofanya kazi ya utafiti wa mbegu kuanzia kwa watafiti wa mwanzo na kuzihakiki, kupitishwa, kuzisajili na baadae kuwafikia wakulima.

Ngwediagi amesema kwa mujibu wa sheria ya mbegu ya mwaka 2003 na marekebisho ya mwaka 2014 pamoja na kanuni za mbegu ya mwaka 2007 na marekebisho ya mwaka 2017 mtafiti anapogundua mbegu mpya anaifanyia utafiti kama inafaa na kisha anaipeleka kwenye taasisi hiyo.

Hivyo Ngwediagi alifafanua kuwa kufuatia kanuni na sheria hizo mtafiti wa awali wa mbegu anatakiwa kutumia muda wa miaka miwili kutafiti na ndipo mbegu hiyo ataifikisha TOSCI ambako itafanyiwa utafiti kwa kipindi cha msimu mmoja wa kilimo na kama inakubalika itaingizwa sokoni.

“Kimsingi TOSCI huwa tunapokea oda za majaribio kutoka kwa watafiti ambao ni wakulima ambao wamefuata sheria na kanuni zetu katika kutafiti mbegu na sisi kitaalamu kunazitafiti ndani ya msimu mmoja wa kilimo na baadae zinapitishwa, lakini kama zikikubalika,” amesema Ngwediagi.

Amesema utafiti huo huchukua muda wa mwaka mmoja TOSCI kufuatia matokeo ya majaribio ya utafiti wa aina mpya ya mbegu kupelekwa kwenye kamati ya taifa ya uidhinishwaji wa mbegu mpya ambayo huishauri kamati ya taifa ya mbegu   kwa ajili ya kutoa mapendekezo.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo alitoa wito kwa watafiti wa umma na binafsi kufanya utafiti wa kutoa aina mpya ya mbegu ya alizeti ambapo inakidhi mahitaji ya watanzania kwani kwa sasa kuna upungufu mkubwa.

Kwa upande wake Mtafiti Msaidizi Idara ya Utafiti na Uendeshaji, Levini Msimbira kutoka taasisi hiyo aliwahamasisha watafiti kuogeza juhudi za utafiti na kupeleka maombi kwa mazao mbalimbali ili kuleta tija katika suala la kilimo na kuwafanya wakulima kuona manufaa ya kilimo.

Amesema kuwa katika utafiti wanaoufanya wameweza kupokea maombi mbalimbali ya utafiti wa mbegu za mazao na wao kuyafanyia kazi na kwamba kwa mwaka 2017 wana aina saba za mbegu za mahindi mapya, pia aina mbili za njugumawe, aina 10 za mahararage na aina tatu za karanga zipo kwenye majaribio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!