Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma
AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the love

WANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani Mara, wameamua kuanza ujenzi wa zahanati kwa nguvu zao, ili kukwepa adha ya kufuata huduma ya afya umbali mrefu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Ofisi ya Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, wanavijiji hao hulazimika kutembea umbali wa kilomita 10 kwenda kupata huduma za afya kwenye Kata jirani ya Murangi.

“Kata ya Musanja yenye vijiji vitatu haina Kituo cha afya wala zahanati hata moja katika vijiji vyake, hii ndio Kata pekee jimboni kwetu yenye hali kama hiyo. Mbunge ameendesha harambee ya ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Mabuimerafuru,” imesema taarifa hiyo.

Kupitia harambee iliyoongozwa na Prof. Muhongo, fedha kiasi cha Sh. 1,350,000 zilikusanywa, mifuko ya saruji 59 na kondoo mbili.

Prof. Muhongo alichangia mifuko 200 ya saruji, ambapo kamati ya ujenzi iliundwa.

Katika hatua nyingine, taarifa hiyo imesema zahanati ya Kijiji cha Nyabaengere, inakaribia kuanza kutoka huduma na kwamba maombi yakufungiwa umeme yamepelekwa TANESCO.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

error: Content is protected !!