Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wanasheria wa Serikali kuanzisha chama chao
Habari za Siasa

Wanasheria wa Serikali kuanzisha chama chao

Spread the love

SERIKALI ina mpango wa kuanzisha Chama cha Wanasheria walio katika utumishi wa Umma. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mpango huo umeelezwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Adelardus Kilangi katika mkutano wa siku mbili wa Mawakili wa Serikali walio  katika utumishi wa umma unaofanyika jijini Dodoma.

Dk. Kilangi wakati akiwasilisha mada kuhusu  Nafasi na Majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa  Mawakili wa Serikali walio  katika utumishi wa umma amesema,  anakusudia  kuanzisha Chama cha Wanasheria walio  katika utumishi wa Umma.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali amebainisha kwamba, kuanzishwa kwa  Chama hicho ni kwa mujibu wa  Ibara ya 74 ya  Muswaada wa  Sheria ya  Marekebisho  Mbalimbali ( Na.2) 2018  inayoeleza kuwa , “ Mwanasheria Mkuu wa Serikali  anaweza  kuanzisha Chama cha Wanasheri katika Utumishi wa Umma”.

Aidha, amesema kuanzishwa kwa  chama cha Mawakili  wa Serikali walio katika utumishi wa Umma hakutawanyima fursa mawakili hao ya  kujiunga au kuwa wanachama wa  vyama  vingine vya kitaaluma kikiwamo Tanganyika law Society ( TLS).

Kuhusu majukumu ya kuitendaji ya chama hicho, Dk. Kilagi ameeleza kuwa Chama hicho kitakuwa  kinakutana  mara moja kwa mwaka kwaajili ya  kujadili masuala mbalimbali ya kisheria ikiwamo  maendeleo ya taaluma hiyo na au kuitishwa na waziri wa katiba na sheria.

Vile vile, amesema Waziri atatunga  Kanuni kuhusu  usimamizi, uongozi, muundo na uendeshaji wa shughuli za chama pamoja na kupokea ripoti ya mikutano ya chama hicho .

Mawakili hao wa Serikali  wapatao mia tisa ( 900) wanatoka  Wizara mbalimbali,  Idara za Serikali, Taasisi na  Mashirika yanayojitegemea, Wakala na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Mkutano huo  ambao  ni wa pili kufanyikia ulifunguliwa na  Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!