Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanafunzi washauriwa kutembelea vivutio vya utalii
Habari Mchanganyiko

Wanafunzi washauriwa kutembelea vivutio vya utalii

Muongoza watalii wa Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, Chalse Karoli, akiwafanunulia jambo, wanafunzi wa Chuo cha Sukari cha Taifa (NSI) kilichopo Kilombero, Mkoani Morogoro.
Spread the love

WANAFUNZI wa ngazi mbalimbali za elimu wametakiwa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo hapa nchini kwa kuwa kufanya hivyo kunawapa fursa ya kutambua uzuri wa nchi, rasilimali zilizopo na kuwaongezea maarifa na uzalendo kwa nchi yao.

Wito huo umetolewa jana tarehe 9 Julai, 2022 na Mhifadhi na Mkuu wa kitengo cha Utalii, Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, Herman Baltazari alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Sukari cha Taifa kilichopo  Kilombero Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro, wakati walipotembelea Hifadhi ya Taifa ya Mikumi.

Baltazar alisema Hifadhi ya Taifa ya Mikumi imejipanga vyema kupokea watalii wa ndani na nje ya nchi hivyo anawakaribisha watanzania wote hususani wanafunzi kutembelea hifadhi hiyo ambayo inafika kwa urahisi.

Naye Kaimu Mkuu wa Chuo cha Sukari Cha Taifa, Aloyce Kasmir, alisema uongozi na wanafunzi wa chuo hicho wameamua kutembelea hifadhi ya Mikumi kwa lengo la  kumuunga Mkono Rais Samia Suluhu Hassan, katika jitihada zake za kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini,lakini pia ni kuwapa fusra wanafunzi wa chuo hicho  cha Sukari cha Taifa kutambua vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Mariam Salumu, mwanafunzi wa kozi ya Teknolojia ya uzalishaji wa sukari wa Chuo cha Sukari cha Taifa, akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wa chuo hicho alisema wamefurahishwa na ziara hiyo kwa kuwa wamepata fursa ya kujifunza kuhusu vivutio vya utalii vilivyopo nchini hususani kwenye Hifadhi ya Taifa ya Mikumi hivyo watakuwa walinzi na mabalozi wa kutangaza rasilimali hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

error: Content is protected !!