Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Michezo Wanafunzi chuo Mwalimu Nyerere wapongezwa kwa ushindi
Michezo

Wanafunzi chuo Mwalimu Nyerere wapongezwa kwa ushindi

Spread the love

 

UONGOZI wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) umewapongeza wanafunzi wanamichezo wa chuo hicho walioshiriki kwenye Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Vyuo Vya Elimu ya Juu Tanzania (SHIMIVUTA) kwa kutwaa kombe la ushindi wa kwanza kitaifa kwenye mchezo wa mpira wa kikapu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza kwenye hafla fupi ya kuwapongeza wanafunzi wanamichezo walioshiriki mashindano ya SHIMIVUTA yaliyomalizika hivi karibuni Jijini Mwanza, Naibu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri wa kitaalamu Prof. Richard Kangalawe ameahidi kuendelea kuwawezesha wanafunzi kwa kuwapatia fursa ya kushiriki mashindano mbalimbali.

Prof. Kangalawe akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa chuo Prof. Shadrack Mwakalila alisema ushindi wa kwanza kitaifa kwenye mchezo wa kikapu ni kitu cha kujivunia na hii itaendelea kuhamasisha wachezaji kujituma zaidi katika mashindano mengine.

Aidha, aliitaja ushindi mwingine ulioletwa na wanamichezo hao kuwa ni pamoja na medali nane kwa wanariadha na michezo mbalimbali.

Kwa upande wake Naibu Mkuu wa Chuo Mipango Fedha na Utawala Dk. Evaristo Haule alisema pamoja na kwamba michezo ni afya lakini ushindi huu umekiheshimisha chuo na kukitangaza.

Aliwataka wanafunzi kutambua namna uongozi unavyowathamini na kuendelea kukua kwenye misingi mema ya maadili kwani ndiyo azma kuu ya chuo.

Hata hivyo, baadhi ya wanafunzi walioshiriki michezo walisema wamefarijika kwa namna chuo kilivyowathamini na kutambua mchango wao na kuahidi ushirikiano wa kutosha kwenye mashindano yajayo huku wakisisitiza wanawake kujitokeza zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Tusua kijanja na mechi za Europa leo

Spread the love  Alhamisi ya leo EUROPA inaendelea ambapo ni mechi za...

Michezo

Hapa Diego Simeone, pale Simeone Inzaghi kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya

Spread the love LIGI ya Mabingwa ulaya itaendelea usiku wa leo ambapoitakwenda...

error: Content is protected !!