Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Wanafunzi chuo Mwalimu Nyerere wapongezwa kwa ushindi
Michezo

Wanafunzi chuo Mwalimu Nyerere wapongezwa kwa ushindi

Spread the love

 

UONGOZI wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) umewapongeza wanafunzi wanamichezo wa chuo hicho walioshiriki kwenye Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Vyuo Vya Elimu ya Juu Tanzania (SHIMIVUTA) kwa kutwaa kombe la ushindi wa kwanza kitaifa kwenye mchezo wa mpira wa kikapu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza kwenye hafla fupi ya kuwapongeza wanafunzi wanamichezo walioshiriki mashindano ya SHIMIVUTA yaliyomalizika hivi karibuni Jijini Mwanza, Naibu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri wa kitaalamu Prof. Richard Kangalawe ameahidi kuendelea kuwawezesha wanafunzi kwa kuwapatia fursa ya kushiriki mashindano mbalimbali.

Prof. Kangalawe akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa chuo Prof. Shadrack Mwakalila alisema ushindi wa kwanza kitaifa kwenye mchezo wa kikapu ni kitu cha kujivunia na hii itaendelea kuhamasisha wachezaji kujituma zaidi katika mashindano mengine.

Aidha, aliitaja ushindi mwingine ulioletwa na wanamichezo hao kuwa ni pamoja na medali nane kwa wanariadha na michezo mbalimbali.

Kwa upande wake Naibu Mkuu wa Chuo Mipango Fedha na Utawala Dk. Evaristo Haule alisema pamoja na kwamba michezo ni afya lakini ushindi huu umekiheshimisha chuo na kukitangaza.

Aliwataka wanafunzi kutambua namna uongozi unavyowathamini na kuendelea kukua kwenye misingi mema ya maadili kwani ndiyo azma kuu ya chuo.

Hata hivyo, baadhi ya wanafunzi walioshiriki michezo walisema wamefarijika kwa namna chuo kilivyowathamini na kutambua mchango wao na kuahidi ushirikiano wa kutosha kwenye mashindano yajayo huku wakisisitiza wanawake kujitokeza zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!