Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani kutuma vifaru 31 nchini Ukraine
Kimataifa

Marekani kutuma vifaru 31 nchini Ukraine

Spread the love

 

SERIKALI ya Marekani imetangaza kutuma vifaru 31 aina ya M1 Abrahams nchini Ukraine, vinavyoelezewa na maafisa wake kuwa bora zaidi duniani, vikiwa vinatosha kwa Serikali ya Ukraine kuunda kikosi kamili cha vifaru. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Uamuzi uliochukuliwa na Marekani jana tarehe 25 Januari 2023 umekuja baada ya wiki kadhaa za mazungumzo na washirika wake wakuu ikiwemo Ujerumani.

Ujerumani nayo jana imetangaza kuipatia Ukraine vifaru 14 aina ya Leopard 2 na kufungua njia kwa washirika wengine pia kutuma vifaru vilivyotengenezwa na Ujerumani.

“Wakati majira ya msimu wa baada ya baridi yanakaribia, jeshi la Ukraine linafanya kazi kulinda eneo wanaloshikilia na kujiandaa kufanya mashambulizi zaidi ili kuikomboa ardhi yao,” Rais Joe Biden alisema jana wakati akitangaza uamuzi wa kutuma vifaru nchini Ukraine zaidi ya miezi 11 baada ya wanajeshi wa kwanza wa Urusi kuingia Ukraine.

Rais Biden alisema Waukraine wanahitaji kuwa na uwezo wa kukabiliana na mbinu na mikakati ya Urusi inayobadilika kwenye uwanja wa vita katika muda wa karibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!