Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanafunzi 716,664 kidato cha kwanza hawajaripoti shuleni hadi sasa
Habari Mchanganyiko

Wanafunzi 716,664 kidato cha kwanza hawajaripoti shuleni hadi sasa

Wanafunzi
Spread the love

IKIWA ni wiki moja tangu kufunguliwa shule nchini Tanzania jumla ya wanafunzi 716,664 wanaopasa kuingia kidato cha kwanza mwaka 2023 bado hawajaripoti na kuandikishwa sawa na asilimia 67. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumapili tarehe 15 Januari, 2023 na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msingwa, wanafunzi 354,277 wakiwemo wenye ulemavu 697, ndiyo waliojiandikisha hadi sasa kati ya wanafunzi 1,070,941 wanaotarajiwa kuingia kidato cha kwanza sawa na asilimia 33 ya matarajio.

Aidha amesema watoto walioandiskishwa kwa aajili ya kuanza darasa la kwanza ni 1,446,067 wakiwemo wenye ulemavu 2,942 saw ana asiliia 88.48 ya matarajio ya kuandikisha watoto 1,634,365.

Msigwa ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote waliochaguliwa kwenda sekondari wanaripoti shuleni.

Amesema Serikali inagharamia elimu ya msingi na Sekondari kwa kutoa Sh 29 bilioni kila mwezi sambamba na kutoa maelekezo mahususi juu ya michango kwa wanafunzi wanaoingia shuleni lengo likiwa ni kuondoa vikwazo vya wanafunzi kujiunga na shule.

Vilevile amesema jumlanya wanafunzi 14,581 wameandikishwa katika Mpango wa Elimu ya Msingi kwa Walioikosa (MEMKWA) na kati ya hao 334 ni wenye mahitaji maalum.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!