Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa
Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the love

Zaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na sekondari Kuriga waliokuwa wametekwa nyara na watu wenye silaha kaskazini magharibi mwa Nigeria mapema mwezi huu wameachiliwa jana Jumapili bila kujeruhiwa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Utekaji nyara huo wa watu wengi huko Kuriga, katika jimbo la Kaduna ulitokea tarehe 7 Machi mwaka huu ikiwamo ni moja ya mashambulizi makubwa kwenye shule kwa miaka kadhaa na kusababisha mjadala nchi humo juu ya ukosefu wa usalama.

Jeshi lilisema kuwa mateka hao waliachiliwa mapema wakati wa operesheni ya ukoaji lakini halikutoa maelezo zaidi.

Msemaji wa jeshi la nchi hiyo, Jenerali Edward Buba alisambaza picha za watoto hao wakiwa wamevalia zare zenye vumbi ndani ya mabasi.

“Mateka waliookolewa ambao ni jumla ya 137 ni pamoja na wanawake 76 na wanaume 61. Waliokolewa katika jimbo la Zamfara na watafikishwa na kukabidhiwa kwa serikali ya jimbo la Kaduna kwa hatua zaidi,” alisema.

Walimu na wakazi awali walisema takriban wanafunzi 280 wenye umri wa kati ya miaka minane na 15 walitekwa nyara wakati wahalifu wenye silaha, wanaojulikana kama majambazi nchini Nigeria, walishambulia shule wakiwa kwenye pikipiki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!