Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wana JOWUTA watakiwa kugombea uongozi, kulipa ada
Habari Mchanganyiko

Wana JOWUTA watakiwa kugombea uongozi, kulipa ada

Katibu wa JOWUTA, Selemani Msuya
Spread the love

 

WANACHAMA wa Chama cha Wafanyakazi wa Vyombo vya habari Tanzania (JOWUTA) wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi za uongozi katika chama hicho huku wakisisitiziwa kulipa ada ili kuwa wagombea wenye sifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rai hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu wa JOWUTA, Selemani Msuya wakati akifungua semina ya siku mbili kwa waandishi wa habari kuhusiana na mabadiliko ya tabianchi iliyoandaliwa na chama hicho chini ya ufadhili wa Shirikisho la Waandishi wa Habari Afrika (IFJ).

Msuya alisema ni muhimu kwa wanachama wa JOWUTA kuwania nafasi za uongozi katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwishoni wa mwezi Novemba huku akisisitiza ili kuweza kuwa mgombea mwenye sifa ni lazima kulipa ada.

“Kila mwanachama hai ambaye atakuwa amelipa ada anayosifa ya kuwania uongozi,  niwaombe tujitokeze kwa wingi tarehe ya uchaguzi  itakayopagwa mwezi Novemba, ili kuweza kupata viongozi bora watakaoendeleza malengo na mambo mazuri yaliyoanzishwa,” alisema Msuya na kuongeza

“JOWUTA ni taasisi iliyosajiliwa na Serikali kwa lengo la kusimamia na kushughulikia matatizo yote yanayowakumba waandishi wa habari hivyo kama viongozi tutaendelea kulisimamia jambo hilo na watakaochaguliwa watalifanyia kazi kwa nguvu zao zote suala hilo,”alisema Msuya.

Hata hivyo Msuya aliwataka waandishi wa habari waliopata fursa ya kuhudhuria mafunzo hayo kujifunza kwa kina kisha kuhabarisha watu juu ya masuala yote yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi.

“Chama hiki kina wanachama wengi lakini kwa siku hizi mbili za mafunzo ni waandishi wachache wamepata bahati kuhudhuria hivyo niwaombe wale wote waliopata nafasi hiyo kujifunza kwa kina na kisha kwenda kuhabarisha  na kuelimisha umma yale yote waliojifunza,” alisema Msuya

Vilevile Msuya aliishukuru IFJ kwa kufadhili mafunzo hayo kwa waandishi wa habari kutoka mikoa mitano Tanzania na kuahidi kuendelea kushirikiana nao katika kuhakikisha kundi hilo linapata mafunzo ya kutosha ya kuwajengea uwezo.

Naye Mwakilishi wa IFJ Afrika, SokhnaDia Coly alitoa wito kwa waandishi wa habari kuongeza ushirikiano ili kukuza taasisi yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!