Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Waislamu washauriwa kusaidia wenye mahitaji
Habari Mchanganyiko

Waislamu washauriwa kusaidia wenye mahitaji

Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Rajabu
Spread the love

WAUNINI wa dini ya Kiislamu nchini wametakiwa kuisaidia jamii yenye uhitaji bila kujali itikadi za kidini, ananadika Dany Tibason.

Hayo yamebainishwa na Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Rajabu muda mfupi baada ya kumalizika ibada ya katika msikiti wa Gadaffi mjini hapa.

Kiongozi huyo wa kiroho amsema ili kufikisha mapenzi ya kiongozi mkuu wa dini hiyo ni lazima ukajua jinsi ya kumtumikia Mungu kwa njia ya utoaji ikiwa ni pamoja na kuwasaidia wenye uhitaji.

Akizungumzia wale wanaokwenda kuhiji amesema wanapokwenda Hija watambue kuwa wanaenda kufanya ibada takatifu na ili kutimiza ibada hiyo ni lazima wanapoondoka wakaacha hakuna malalamiko wala manung’uniko ya aina yoyote.

“Wale wote wanaoenda Hija ni lazima wakatambua kuwa wanakwenda katika ibada muhimu kweli kweli na ili kuweza kutimiza malengo ni jambo la msingi sana kuziacha familia au majirani wakiwa na furaha na hakuna malalamiko ya aina yoyote” amesema Sheikh Rajabu.

Aidha, ametoa wito kwa waumini wote wa dini hiyo kuhakikisha wanafanya maombi ya kuliombea taifa pamoja na viongozi mbalimbali ili amani na uchumi viwepo na iwe faraja kwa Watanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!