Sunday , 3 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Kampuni ya Wakili Fatuma Karume yapigwa mabomu
Habari MchanganyikoTangulizi

Kampuni ya Wakili Fatuma Karume yapigwa mabomu

Sehemu ya ofisi ya Wakili Fatma Karume ilivyoteketea kwa moto
Spread the love

KAMPUNI ya Mawakili ya IMMMA ya jijini Dar es Salaam, imevamiwa na watu wasiojukana na kulipuliwa kwa mabomu usiku wa kuamkia leo, anaandika Faki Sosi.

Jengo hilo lililopo eneo la Upnaga jijini Dar es Salaam lilikumbwa na mkasa huo usiku wa kuamkia leo, ambapo mabomu hayo yalibomoa madirisha, vioo kupasuliwa, mageti kuvunjwa pamoja ukuta kutobolewa.

Mmoja wa Wakurugenzi wa kampuni hiyo, Sadock Magai akizungumza na waandishi wa habari, alikiri kutokea uvamizi huo, lakini akasema hakuna mali iliyoibiwa ndani.

Magai anasema kuwa hawajajua kama kuna nyaraka zimepotea lakini kwa haraka walioangalia hakuna kitu kilichochukuliwa.

https://www.youtube.com/watch?v=veciCsG4CRg

Imeelezwa kuwa hiyo ni kampuni anayofanyia kazi Wakili maarufu nchini Fatuma Karume ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa Zanzibar.

Kampuni hiyo inamilikiwa na Mawakili maarufu hapa nchini na mpaka sasa haijajulikana lengo la uvamizi huo ilikuwa ni kutaka kuiba vitu ama kudhuru wafanyakazi wake.

Jengo hilo limezingirwa na makachero wa Jeshi la Polisi ambao wameanza kufanya uchunguzi wao kuanzia mapema leo asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Habari Mchanganyiko

TARURA kujenga madaraja 189 kwa teknolojia ya mawe

Spread the loveWakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imejipanga kujenga...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

error: Content is protected !!