Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kampuni ya Wakili Fatuma Karume yapigwa mabomu
Habari MchanganyikoTangulizi

Kampuni ya Wakili Fatuma Karume yapigwa mabomu

Sehemu ya ofisi ya Wakili Fatma Karume ilivyoteketea kwa moto
Spread the love

KAMPUNI ya Mawakili ya IMMMA ya jijini Dar es Salaam, imevamiwa na watu wasiojukana na kulipuliwa kwa mabomu usiku wa kuamkia leo, anaandika Faki Sosi.

Jengo hilo lililopo eneo la Upnaga jijini Dar es Salaam lilikumbwa na mkasa huo usiku wa kuamkia leo, ambapo mabomu hayo yalibomoa madirisha, vioo kupasuliwa, mageti kuvunjwa pamoja ukuta kutobolewa.

Mmoja wa Wakurugenzi wa kampuni hiyo, Sadock Magai akizungumza na waandishi wa habari, alikiri kutokea uvamizi huo, lakini akasema hakuna mali iliyoibiwa ndani.

Magai anasema kuwa hawajajua kama kuna nyaraka zimepotea lakini kwa haraka walioangalia hakuna kitu kilichochukuliwa.

https://www.youtube.com/watch?v=veciCsG4CRg

Imeelezwa kuwa hiyo ni kampuni anayofanyia kazi Wakili maarufu nchini Fatuma Karume ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa Zanzibar.

Kampuni hiyo inamilikiwa na Mawakili maarufu hapa nchini na mpaka sasa haijajulikana lengo la uvamizi huo ilikuwa ni kutaka kuiba vitu ama kudhuru wafanyakazi wake.

Jengo hilo limezingirwa na makachero wa Jeshi la Polisi ambao wameanza kufanya uchunguzi wao kuanzia mapema leo asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!