Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waganga 11 mbaroni kwa kuagua bila kibali
Habari Mchanganyiko

Waganga 11 mbaroni kwa kuagua bila kibali

Spread the love

Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limewakamata watuhumiwa 11 kwa kufanya shughuli za uganga bila kuwa na kibali. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Taarifa iliyotolewa na leo Alhamis Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Thoepista Mallya imesema watuhumiwa hao wakamatwa kutokana na operesheni iliyofanywa na jeshi hilo tarehe 9 Januari mwaka huu.

Amewataha watuhumiwa hao kuwa ni Chifu wa kabila la Kinyiha aitwaye Mwene Nzunda (44) mkazi wa kiji cha Nambala pamoja na wenzake ambao ni Anthony Yatilinga Mapumba (G5) mkazi wa llembo, Isambi Yasinta Mghallah (80) mkazi wa Majengo, Kostebo Ngawelo Mziho (53) mkazi wa Nambala.

RPC Songwe

Wengine ni Tamimu Balison Mdolo (57) mkazi wa lembo, Biton Daimon Nzunda (64) Balozi mtaa wa Nsenya Shina namba 8 na mkazi wa Nsenya, Amnos Nzunda (23) Steven Mwilenga (46) David Frank Mapumba (72) mkazi wa llembo, George Greyson Mghala (43) mkulima, mkazi wa mtaa wa Danida katika kijiji cha llembo na Jailos Sola (42) mkulima na mkazi wa Mbimba.

Kwa melezo ya watuhumiwa hao wanasema kwamba katika kiji hicho kuna mambo yanayofanyika yanayoashiria kuwa ni yakishirikina.

Aidha amesema Jeshi la Polisi linakamilisha upelelezi wa kesi hi ili watuhumiwa waweze kufikishwa mahakamani.

“Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Songwe kuwa ni marufuku kwa mtu yoyote kufanya shughuli za uganga bila kibali ikiwa ni pamoja na kitendo cha kusafisha nyumba zinazodhaniwa kuwa na uchawi kwani kitendo hicho kinaleta chuki na udhalilishaji kwa jami.

“Pia kwa mtu yoyote anapotaka kufanya kusanyiko lolote ni lazima viongozi wa sehemu husika wajulishwe,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara yaomba bajeti ya Sh. 67.9 bilioni, wamachinga watengewa bilioni 10

Spread the loveBAJETI ya Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na...

Habari MchanganyikoTangulizi

Migogoro ya ndoa yaongezeka, Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveMIGOGORO ya ndoa na familia imeongezeka kwa asilimia 8.3  kutoka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yahamasisha uanzishaji vituo vya kulea watoto wachanga

Spread the loveSERIKALI imewahimiza wananchi kujenga vituo vya kulelea watoto wadogo na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

error: Content is protected !!