KAMPUNI ya Vodacom Tanzania imewazawadia mawakala wa usajili wa (Freelancer) ya jiko la gezi na mtungi wake ikiwa ni sehemu ya kampeni yake ya ‘Loyalty Program’ ambayo inalenga kuboresha maslahi ya mawakala wa usajili nchini kote. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kampeni hiyo ya ‘Loyalty Program’ mbali na zawadi ya jiko la gesi na mtundi wake pia inatoa zawadi kama vile bima ya afya, pikipiki, luninga, simu za mkononi, magodoro, pesa taslimu na ikiwemo safari itakayogharamiwa kila kitu ya kwenda nchini Afrika ya Kusini mwezi Oktoba 2023.
Kupitia kampeni hiyo Vodacom imewazawadia mawakala wawili wa jijini Dar es Salaam ambao wamefanya vizuri katika shughuli zao za usajili na kujikusanyia pointi nyingi, mawakala hao ni Goodluck Clement na Mathias Lutumbi.
Msimamizi wa Mauzo wa Vodacom Tanzania, Iddy Chitanda (kulia) akimkabidhi wakala wa usajili Goodluck Clement (kushoto) zawadi ya jiko la gesi na mtungi wake baada ya kujikusanyia pointi nyingi kwa kusajili wateja wapya wengi na wateja hao kununua salio na vifurushi kupitia M-Pesa.
Msimamizi wa Mauzo wa Vodacom Tanzania, Iddy Chitanda (kulia) akimkabidhi wakala wa usajili Mathias Lutumbi (kushoto) zawadi ya jiko la gesi na mtungi wake baada ya kujikusanyia pointi nyingi kwa kusajili wateja wapya wengi na wateja hao kununua salio na vifurushi kupitia M-Pesa.
Msimamizi wa Mauzo wa Vodacom Tanzania, Iddy Chitanda (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na mawakala wa usajili wa kampuni hiyo Mathias Lutumbi (kulia) na Goodluck Clement (kushoto) mara baada ya kuwakabidhi zawadi za majiko ya gesi na mitungi yake baada ya kujikusanyia pointi nyingi kila baada ya mteja mpya aliyemsajili akinunua salio na bando kwa M-Pesa.
Leave a comment