Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia
MichezoTangulizi

Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia

Spread the love

 

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameitaka klabu ya Yanga kumaliza tofauti zake na mchezaji wake wa kutumainiwa Feisal Salum ‘Fei Toto.’ Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Akizungumza katika hafla ya kupongeza timu hiyo, kwa kushinda mchezo wake wa pili wa fainali Jumamosi iliyopita, nchini Algeria, leo Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Samia alisema, hafurahishwi kuona Yanga inaendeleza mgogoro na mchezaji wake.

“Klabu ya Yanga ni kubwa sana. Ni aibu kuendeleza magomvi na wachezaji wake. Naomba hili la Fei Toto, kalimalizeni na nasubiria mrejesho,” alisisitiza Rais Samia.

Fei Toto aliondoka Yanga kuanzia mwishoni mwa mwaka jana, baada ya kudai kuwa anahitaji maslahi zaidi, akavunja mkataba kwa kuweka kiasi cha Sh. 112 milioni kwenye akaunti ya klabu hiyo, kwa lengo la kuvunja mkataba wake.

Hata hivyo, Kamati ya Sheria Hadhi za Wachezaji iliyopo chini ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ilieleza kuwa mchezaji huyo bado ni mali ya Yanga kwa kuwa hakufuata taratibu za kuvunja mkataba wake.

Kwa muda sasa, mchezaji huyo amekuwa akihaha kutaka kuondoka ndani ya klabu hiyo, lakini juhudi zake zimekuwa zikigonga mwamba, baada ya vyombo vinavyoongoza michezo kuelekeza kuwa Feisal Salim, anapaswa kufanya majadiliano na klabu yake, kabla ya kuvunja mkataba

Haijaweza kufahamika mara moja, iwapo Fei Toto atarejea Yanga au ataruhusiwa kuondoka. Ombi la Dk. Samia kutaka Yanga kumalizana na Fei Toto, halikueleza pande hizo mbili kuchukua hatua gani.

Katika hafla hiyo, viongozi mbalimbali wa michezo, akiwamo Ledger Tenga, mwenyekiti wa Baraza la Michezo la taifa (BMT); Wallace Karia, rais wa shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF); mhandishi Hersi Said; Murtaza Mangungu, Mwenyekiti wa Simba na Ghalib Said Mohamed, mfadhili mkuu wa Yanga, walihudhuria hafla hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za SiasaTangulizi

Makonda awapopoa wanaomtofautisha Magufuli na Samia

Spread the loveKATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),...

error: Content is protected !!