Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Vituo vya ukaguzi mabasi ya umma vyaandaliwa
Habari Mchanganyiko

Vituo vya ukaguzi mabasi ya umma vyaandaliwa

Spread the love

SERIKALI kupitia Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani limeandaa utaratibu wa kuwa na vituo maalum vya ukaguzi vya mabasi ya umma. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 23 Aprili 2019 bungeni na Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani alipokuwa akijibu swali la Rose Tweve (CCM).

Katika swali lake, Rose alitaka kujua ni lini serikali itaanza utaratibu wa kuwa na vituo maalum vya ukaguzi vya mabasi ikiwemo daradara?

Masauni amesema, vituo hivyo vitakuwa vituo vikuu vya mabasi yote katika kila mkoa, ambapo mabasi ya abiria hukaguliwa kabla ya kuanza safari na pale yanapofika mwisho wa safari.

Amesema, ukaguzi wa pembezoni mwa barabara ambao huhusisha mabasi ya daladala na vyombo vingine vya moto, hufanyika katika vituo vya ukaguzi maalum ambavyo vipo katika barabara kuu na katika barabara zingine za miji na majiji.

Amesema, Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168 iliyorejewa 2002 kifungu 81, kinampa uwezo Askari Polisi kulisimamisha gari lolote barabarani au sehemu yoyote anapolitilia shaka na kulikagua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!