Sunday , 3 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Vituo vya ukaguzi mabasi ya umma vyaandaliwa
Habari Mchanganyiko

Vituo vya ukaguzi mabasi ya umma vyaandaliwa

Spread the love

SERIKALI kupitia Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani limeandaa utaratibu wa kuwa na vituo maalum vya ukaguzi vya mabasi ya umma. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 23 Aprili 2019 bungeni na Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani alipokuwa akijibu swali la Rose Tweve (CCM).

Katika swali lake, Rose alitaka kujua ni lini serikali itaanza utaratibu wa kuwa na vituo maalum vya ukaguzi vya mabasi ikiwemo daradara?

Masauni amesema, vituo hivyo vitakuwa vituo vikuu vya mabasi yote katika kila mkoa, ambapo mabasi ya abiria hukaguliwa kabla ya kuanza safari na pale yanapofika mwisho wa safari.

Amesema, ukaguzi wa pembezoni mwa barabara ambao huhusisha mabasi ya daladala na vyombo vingine vya moto, hufanyika katika vituo vya ukaguzi maalum ambavyo vipo katika barabara kuu na katika barabara zingine za miji na majiji.

Amesema, Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168 iliyorejewa 2002 kifungu 81, kinampa uwezo Askari Polisi kulisimamisha gari lolote barabarani au sehemu yoyote anapolitilia shaka na kulikagua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Habari Mchanganyiko

TARURA kujenga madaraja 189 kwa teknolojia ya mawe

Spread the loveWakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imejipanga kujenga...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

error: Content is protected !!