Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ulanga wapigwa msasa kuhusu elimu ya sheria
Habari Mchanganyiko

Ulanga wapigwa msasa kuhusu elimu ya sheria

Spread the love

KATIKA kuadhimisha wiki ya sheria nchini, Mahakama ya Wilaya Ulanga imetoa elimu ya sheria kwa wadau mbalimbali kwa lengo la kuwaelimisha kuhusu masuala ya maadili na malezi bora kwa  watoto. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Akizungumza katika kilele cha Siku ya Sheria nchini wilaya ya Ulanga leo Alhamisi, Hakimu Mkazi Mfawidhi mahakama ya wilaya hiyo, Christopher Bwakila amesema katika kutoa elimu hiyo, watumishi wa mahakama hiyo na wadau wake walijigawa katika makundi matatu.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Ulanga, Christopher Bwakila (kushoto) wengine ni DC wa Ulanga na DAS.

“Tulitembelea shule za Sekondari (mfano Kwiro Boys, Lupiro, Celina Kombani, Mwaya, Nawenge): Shule za msingi (Mahenge A na Mahenge B) ambapo kamati ya uelimishaji ilifanikiwa kufanya mkutano na wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika shule hizo kwa lengo la kuwaelimisha kuhusu masuala mbalimbali yakiwemo masuala ya maadili na malezi  bora  kwa  watoto.

“Pia tulifanya mikutano maeneo  mbalimbali  yenye mikusanyiko kama vile Soko la Lupiro na Mahenge, Mawasiliano, Safari Road, Mwaya Center, Ilonga, Chikuti, Idunda, kwenye vituo vya bodaboda (Hospitali ya Wilaya Ulanga, Togo, Stone na Stendi),” amesema.

Aidha, amesema kwa niaba ya kamati iliyohusika na utoaji elimu na Mahakama kwa ujumla amemshukuru Mratibu Elimu Kata ya Mahenge Mjini pamoja na Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari ambazo kamati ya elimu ilitembelea na kuendesha mkutano.

“Bila kuwasahau viongozi wote wa Kata na Vijiji ambao kamati ilitembelea maeneo yao na kufanya mikutano ya utoaji elimu ambapo walitusaidia kuwataarifu wananchi kuhusu ujio wetu,” amesema.

Ameongeza kuwa mahakama ya Tanzania imekuwa ikiadhimisha wiki na siku ya sheria kila mwanzoni mwa mwaka na mwaka huu wa 2024, kuanzia tarehe 24 Januari 2024 hadi 30 Januari 2024 wananchi walipata elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kisheria.

Amesema ana imani kuwa elimu waliyoitoa wakati wa wiki ya sheria itawasaidia sana wananchi kwa sababu wananchi wengi walionyesha kuridhika na elimu iliyotolewa na kutamani utoaji wa elimu uwe endelevu.

“Napenda kuwahakikishia elimu hii itakuwa endelevu kwakuwa itakuwa inatolewa Mahakamani asubuhi kabla ya kuanza shughuli za Mahakama.

“Leo tunafikia kilele cha siku ya sheria nchini ambapo maadhimisho ya mwaka huu, yanaongozwa na kauli mbiu isemayo. “Umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa taifa: nafasi ya mahakama na wadau katika kuboresha mfumo jumuishi wa haki jinai”.

Amesema kauli mbiu ya mwaka huu kwenye siku na wiki ya sheria imekuja katika kipindi sahihi kwa sababu kwa sasa Mahakama ya Tanzania inatekeleza Mpango Mkakati wa miaka mitano wa awamu ya pili (2020/21- 2024/25)   ambapo   kuna   maboresho   mbalimbali.

“Maboresho hayo yanaendelea kutekelezwa na Mahakama ili kuendana na nguzo tatu za mpango mkakati huo ambazo nitazielezea katika hotuba hii. Lengo kuu la kutekeleza Mpango Mkakati huu ni kuhakikisha Mahakama ya Tanzania inafikia lengo lake kuu ambalo ni utoaji wa haki kwa wakati na kwa watu wote,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!