Tuesday , 30 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Uhaba wa  maji pasua kichwa kwa serikali
Habari Mchanganyiko

Uhaba wa  maji pasua kichwa kwa serikali

Wananchi wakiwa kaitka sehemu yemye Uhaba wa maji
Spread the love

SERIKALI imesema imeifanya  tathmini ya miradi ya maji yote nchini na kwa sasa inawekewa mipango sahihi ya kutekelezwa ili wananchi waweze kupata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa, anaandika Dany Tibason.

Kauli hiyo imetolewa leo  mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo alipokuwa akijibu maswali ya Mbunge wa Monduli Julius Laizer (Chadema).

Katika swali lake, Mbunge huyo alihoji ni lini serikali itatekeleza ahadi ya Rais aliyoitoa wakati wa kampeni za Uuchaguzi Mkuu 2015 kuhusu ukarabati wa Mabwawa matatu ili wananchi wa Esilalei waweze kupata maji kwa ajili ya mifugo yao.

Akijibu maswali hayo,  Jafo alisema serikali katika mwaka wa fedha 2016/17 imekamilisha usanifu kwa ajili ya ukarabati wa Mabwawa ya Joshoni na Olkuro ili kubaini kuwa Sh.Bilioni 1.45 zinahitajika kwa kazi hiyo.

Alisema mahitaji hayo yatazingatiwa katika mipango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
Aidha alisema serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji katika vijiji vya Lendikinya kata ya Sepeko ambao unatekelezwa kwa gharama ya Sh.Milioni 868.07.

“Kazi imefikia asilimia 35 na itakamilika mwezi Oktoba 2017 kwa kuzingatia mkataba na mwaka 2017/18 serikali imeidhinisha Sh.Milioni 639.5 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Nanja,”alisema Jafo.

Kadhalika, alisema lengo la kufanya tathmini hiyo ni kujua nini kilichokwamisha baadhi ya miradi ili serikali iweze kutatua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wenye ulemavu waiomba MISA-TAN iwajengee uwezo wa uhuru wa kujieleza

Spread the love  TAASISI ya vyombo vya Habari kusini mwa Afrika (MISA-TAN)...

Habari Mchanganyiko

Wanawake wajawazito 2000 Korogwe washiriki Marathon, Mwenyekiti UWT amsifu Jokate

Spread the loveWANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki...

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

error: Content is protected !!