BARAZA la Habari Tanzania (MCT), leo tarehe 11 Oktoba 2019 limezindua rasmi usaili wa kuwania tuzo za umahiri wa uandishi wa habari (EJAT) kwa mwaka 2019. Anaripoti Martin Kamote … (endelea).
Baraza hilo limehimiza waandishi wa habari za mitandao, kujitokeza kwa wingi huku likiongeza makundi matatu mapya ya tuzo na kuwa 20.
Makundi toka 17 ya awali ni habari za hedhi salama, uandishi wa habari za ubunifu na maendeleo ya watu pia habari za afya ya uzazi.
Kajubi Mukajanga, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya EJAT amesema, makundi yaliyoshindaniwa mwaka jana na sasa hayatokuwepo ni habari za usalama na ubora wa chakula, habari za kodi na mapato pamoja na habari za afya kwa kuwa, yamekosa wadhamini.
Leave a comment