Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tuzo EJAT zazinduliwa, makundi matatu yatemwa
Habari Mchanganyiko

Tuzo EJAT zazinduliwa, makundi matatu yatemwa

Kajubi Mukajanga, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya EJAT
Spread the love

BARAZA la Habari Tanzania (MCT), leo tarehe 11 Oktoba 2019 limezindua rasmi usaili wa kuwania tuzo za umahiri wa uandishi wa habari (EJAT) kwa mwaka 2019. Anaripoti Martin Kamote … (endelea).

Baraza hilo limehimiza waandishi wa habari za mitandao, kujitokeza kwa wingi huku likiongeza makundi matatu mapya ya tuzo na kuwa 20.

Makundi toka 17 ya awali ni habari za hedhi salama, uandishi wa habari za ubunifu na maendeleo ya watu pia habari za afya ya uzazi.

Kajubi Mukajanga, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya EJAT amesema, makundi yaliyoshindaniwa mwaka jana na sasa hayatokuwepo ni habari za usalama na ubora wa chakula, habari za kodi na mapato pamoja na habari za afya kwa kuwa, yamekosa wadhamini.

Tuzo hizo zimedhaminiwa na Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISATAN), Wakfu wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA).
Wengine ni Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), HakiElimu, Sikika, Agriculture Non_State ASctors Forum (ANSAF) na Chama cha Wamiliki wa Vyombo Vya Habari Tanzania (MOAT).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!