Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Tukikukamata tutakutandika faini – DED Temeke
Habari Mchanganyiko

Tukikukamata tutakutandika faini – DED Temeke

Spread the love

 

MTU yeyote atakayekamatwa akitupa takataka katika Mamispaa ya Temeke, jijini Dar es Salaam, atatozwa faini.Anaripoti Brightness Boaz, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 27 Januari 2021, na Lusubilo Mwakabibi, Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke mbele ya waandishi wa habari ofisini kwake.

Amewataka wakazi wa manispaa hiyo na wale wanaotumia barabara ndani ya manispaa yake, kuhakikisha wanaweka mazingira safi sambamba na utunzaji wa barabara.

“Tumetengeneza barabara za kisasa ili zichukue miaka mingi ijayo, hatutakubali Temeke kuwa eneo la kutupa takataka barabarani.

“Mtanzamia yeyote atakayepanda daladala, bodaboda, bajaji au usafiri binafsi, ukionekana umetupa takataka yoyote utakamatwa na kutandikwa faini,” amesema Mwakabibi.

Pia mkurugenzi huyo amewataka wakazi wa manispaa huyo kulipia ushuru wa takataka katika magari yanayofanya kazi ya kukusanya taka hizo.

1 Comment

  • Asante mkurugezi kwa kauli njema lakini tunakuomba utuweke sehem ya kuifadhi taka mitaani na sehem za wazi ukiwa utayatimiza hapo kweli mtupa taka ovyo anastaili kuchukuliwa hatua za kisheria

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!