Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo TFF yamfungia Kuuli kutojihusisha na soka
Michezo

TFF yamfungia Kuuli kutojihusisha na soka

Wakili Revocutus Kuuli
Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia kamati ya maadili imemfungia maisha kujihusisha na soka aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Wakili Revocutus Kuuli baada ya kukutwa na hatia ya makosa matatu ya kimaadili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Makosa hayo ambayo ni kusambaza nyaraka za TFF kwa watu ambao haziwahusu ambapo ni kinyume na utaratibu wa taasisi hiyo, kutoa maelezo yanayoonesha kuwa na mgangano wa kimaslahi na kufanya vitendo vinavyopelekea kulishusha hadhi shirikisho hilo.

Akisoka uwamuzi huo Mwenyekiti wa kamati ya maadili kwenye shirikisho hilo Wakili Hamidu Mbwezeleni ameeleza kuwa makosa hayo yote matatu yanastahili adhabu hiyo ya kutojihusisha na masuala ya mpira wa miguu na hakuna aliyeonewa.

“Uamuzi huu umechukuliwa kwa kufuata kanuni na taratibu. Hakuna aliyemuonea Kuuli niliweke hilo sawa,” alisema Wakili Mbwezeleni.

Ikumbukwe Kuuli alijiuzuru nafasi hiyo ikiwa siku chache baada ya katibu Mkuu wa Tff Wilfred Kidao kumwandikia barua ya kujieleza ndani ya siku tatu kwanini alisimamisha uchaguzi wa klabu ya Simba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!