Tuesday , 21 March 2023
Home Kitengo Michezo TFF yamfungia Kuuli kutojihusisha na soka
Michezo

TFF yamfungia Kuuli kutojihusisha na soka

Wakili Revocutus Kuuli
Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia kamati ya maadili imemfungia maisha kujihusisha na soka aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Wakili Revocutus Kuuli baada ya kukutwa na hatia ya makosa matatu ya kimaadili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Makosa hayo ambayo ni kusambaza nyaraka za TFF kwa watu ambao haziwahusu ambapo ni kinyume na utaratibu wa taasisi hiyo, kutoa maelezo yanayoonesha kuwa na mgangano wa kimaslahi na kufanya vitendo vinavyopelekea kulishusha hadhi shirikisho hilo.

Akisoka uwamuzi huo Mwenyekiti wa kamati ya maadili kwenye shirikisho hilo Wakili Hamidu Mbwezeleni ameeleza kuwa makosa hayo yote matatu yanastahili adhabu hiyo ya kutojihusisha na masuala ya mpira wa miguu na hakuna aliyeonewa.

“Uamuzi huu umechukuliwa kwa kufuata kanuni na taratibu. Hakuna aliyemuonea Kuuli niliweke hilo sawa,” alisema Wakili Mbwezeleni.

Ikumbukwe Kuuli alijiuzuru nafasi hiyo ikiwa siku chache baada ya katibu Mkuu wa Tff Wilfred Kidao kumwandikia barua ya kujieleza ndani ya siku tatu kwanini alisimamisha uchaguzi wa klabu ya Simba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!