Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Dk. Ndugulile amweka ndani Mganga Mkuu
Afya

Dk. Ndugulile amweka ndani Mganga Mkuu

Spread the love

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile ameagiza Jeshi la Polisi wilayani Mbulu mkoa wa Manyara, kuwaweka ndani Mganga Mkuu wa wilaya hiyo, Dk. Joseph Foma na Mhandisi wa ujenzi wa kituo cha afya, Mhandisi Samweli Bundala. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Dk. Ndugulile ameagiza mganga huyo kuwekwa ndani baada ya kukagua ujenzi huo na kubaini mapungufu ya kitaalam katika ujenzi wa kituo hicho kilichopo kata ya Dongobeshi wilayani Mbulu.

Katika ukaguzi huo, Dk. Ndugulile alibaini madudu katika kituo hicho, kwa kukuta makosa ya kiufundi kwenye eneo la upasuaji na sehemu ya kuifadhi maiti.

‘’Kamanda mkuu wilaya weka ndani wote wawili akili iwakae sawa inakuwaje mhandisi unakaa eneo la ujenzi bila kuwa na ramani ya ujenzi na mganga mkuu unashindwa kutoa ushauri kwa wataalamu wa ujenzi kujenga kituo cha afya bila kuzingatia vigezo vya kitaaluma katika ujenzi wa eneo la upasuaji,” alisema Dk. Ndugulile.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!