Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko TBA: Taasisi za fedha zisiwaache nyuma wanawake
Habari Mchanganyiko

TBA: Taasisi za fedha zisiwaache nyuma wanawake

Spread the love

CHAMA cha  Mabenki Tanzania (TBA)  kimetoa wito kwa taasisi za kifedha nchini kuhakikisha kuwa makundi yote kwenye jamii hususani wanawake ushirikishwaji wao unapewa kipaumbele. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mwenyekiti wa Chama cha Mabenki Tanzania (TBA) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya Taifa (NBC), Theobald Sabi akitoa hotuba kwa washiriki wa maadhimisho ya siku ya wanawake kutoka sekta za kibenki katika hafla iliyofanyika jana Jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyofanyika jana tarehe 16Machi 2023 jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Chama cha Mabenki Tanzania (TBA) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya Taifa (NBC), Theobald Sabi alisema ni muhimu kwa taasisi za kifedha kuhakikisha kunakuwa na ushirikishwaji wa wanawake kwenye huduma za kibenki au kifedha nchini.

“Tunatambua kuwa wanawake ni sehemu kubwa ya jamii yetu, zaidi ya asilimia 51 ya watanzania wote ni wanawake na kwa hivyo ni muhimu tunapoongeza ujumuishwaji wa kifedha kwenye jamii kundi la wanawake lisiachwe nyuma,”  amesema Sabi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Mabenki Tanzania (TBA), Tusekelege Joune akitoa hotuba  ya ufunguzi wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa liyofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Sabi amebainisha kuwa kwa upande wa benki ya NBC wameanza na wafanyakazi wakijaribu kuhakikisha kuwa kama benki wanakuwa na sera rafiki kwa wanawake ili waweze kufikia malengo yao ya kikazi, kiajira, na kiuchumi.

Aidha naye Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Mabenki Tanzania (TBA), Tusekelege Joune amesema inatia hamasa kuona kuwa benki nyingi nchini zimekuwa mstari wa mbele kubuni bidhaa mbalimbali ambazo zimekuwa maalum katika kukidhi mahitaji ya wanawake nchini.

Mwenyekiti wa Chama cha Mabenki Tanzania (TBA) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya Taifa (NBC), Theobald Sab akisaliamiana na Mkurungezi wa Benki ya Equity Tanzania, Isabela Maganga katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani iliyofanyika katika hoteli ya Onomo jijini Dar es Salaam jana.

“Tunashukuru kuwa benki zimekuwa mstari wa mbele katika kuja na bidhaa mbalimbali ambazo zimekuwa mahsusi kwa ajili ya wanawake nchini ikiwamo wafanyabiashara, akihitaji huduma za kibenki anakutana na bidhaa ambayo imeandaliwa kwa ajili ya kukidhi mahitaji yake,” amesema Joune.

Joune ameongeza kuwa maadhimisho hayo ya Siku ya Wanawake Duniani kwa upande wa sekta ya kibenki kumekua na ongezeko kwa  benki kuja na huduma ya dhamana maalum kwa ajili ya wanawake.

Pia kumetolewa hati fungani kwa ajili ya maendeleo ya wanawake ikiwa ni jitihada mbalimbali zinazofanywa na sekta hiyo katika kuinua wanawake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!