PUTO la kijasusi la China limetajwa kuwa halikuweza kusababisha tishio la usalama nchini Marekani badala yake limeweza kugundua udhaifu wa kijeshi Marekani imeripotiwa na mtandao wa AlwaysFirst. Inaripoti Mitandao ya Kijamii … (endelea).
Puto hilo liliibua mjadala wa masuala ya usalama kidunia hivi karibuni lilielezwa kuwa lilikuwa likipeleleza anga ya Marekani lilikuwa na China.
Watetezi wa China kwenye mgogoro huo wanawasiwasi kuwa majukwaa ya upelelezi ya nchi hiyo yataharibiwa
Wasiwasi huo unatokana na kitendo cha China kurusha puto la kijasusi katika anga la Marekani na kuibua hisia tofauti na kufanya uhusiano wa nchi hizo mbili uzidi kuteteleka.
Licha ya Jeshi la China kuwa na makombora ya masafa marefu lakini wachambuzi wanadai kuwa makombora hayo si chochote kwa kuwa setalaiti zao zinashindwa kufika masafa hayo ndiyo wakaanzisha mpango wa puto la anga la kijasusi ambapo moja lishalipasuliwa kwenye anga ya Marekani.
Puto la Kijasusi la China limetajwa kuwa na uwezo wa kufikia sehemu muhimu za Marekani kama vile kituo cha Malmstrom.
Wakati Washington iliashiria Beijing kwamba ilichukua uvamizi huo kwa uzito kwa kupeleka mifumo yake ya juu zaidi ya silaha ili kulitungua puto hilo, China wameonyesha utayari wao juu ya shari ya vita kwa kuongeza asilimi 7.2 zaidi kwenye bajeti ya Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo.
Mzozo huu umepelekea uhusiano wa mataifa haya kuwa mbaya zaidi.
Leave a comment