Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania yaripoti kifo cha kwanza mgonjwa wa Corona
Habari MchanganyikoTangulizi

Tanzania yaripoti kifo cha kwanza mgonjwa wa Corona

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeripoti kifo cha kwanza cha Mgonjwa wa Homa Kali ya Mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19). Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Taarifa ya kifo hicho imetolewa leo tarehe 31 Machi 2020 na Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Taarifa ya Waziri Ummy inaeleza kuwa, kifo hicho kimetokea alfajiri ya leo katika Kituo cha Matibabu ya Wagonjwa wa COVID-19, kilichopo Mloganzila jijini Dar es Salaam.

Waziri Ummy amesema marehemu alikuwa mwanaume mwenye umri wa miaka 49, ambaye alikuwa anasumbuliwa na maradhi mengine.

“Ninasikitika kutangaza kifo cha kwanza cha mgonjwa wa COVID-19 hapa nchini kilichotokea alfajiri ya leo katika kituo cha matibabu ya wagonjwa wa COVID-19 kilichopo Mloganzila. Marehemu ni Mtanzania  ambaye pia alikuwa anasumbuliwa na maradhi mengine,” inaeleza taarifa ya Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amesema hadi kufikia leo idadi ya wagonjwa wa COVID-19 nchini ni 19, ambapo aliyepona ni mmoja na aliyefariki dunia mmoja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!