IDADI ya wagonjwa wa Homa Kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19), nchini Tanzania wamefika 19. Inaripoti Regina Mkonde…(endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 30 Machi 2020 na Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
Waziri Ummy amesema, wagonjwa watano wapya, watatu wanatoka jijini Dar es Salaam na wawili wanatoka visiwani Zanzibar.
“Ninapenda kutoa taarifa kwamba leo tumethibitisha kuwepo kwa wagonjwa wapya watano wa COVID-19, baada ya kufanyiwa vipimo katika maabara yetu Kuu ya Taifa, Hivyo sasa jumla ya wagonjwa wa COVID-19 nchini ni 19,” amesema Waziri Ummy.
Akitoa ufafanuzi wa wagonjwa hao, Waziri Ummy amesema mmoja mwanaume mwenye umri wa miaka 49 alipata maradhi hayo baada ya kukutana na raia wa kigeni aliyetoka nchi zilizoathirika zaidi. Wakati mwingine ni mwanamke mwenye umri wa miaka 21.
“Mwingine ni mwanaume mwenye umri a miaka 49, Mtanzania ambae pia ni miongoni mwa watu waliokuwa wakifuatiliwa,” amesema Waziri Ummy.
Leave a comment