Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania kuzindua mfumo wa biashara, duka la kidigitali
Habari Mchanganyiko

Tanzania kuzindua mfumo wa biashara, duka la kidigitali

Prof. Kitila Mkumbo
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, iko mbioni kuzindua nembo maalumu itakayotambulisha bidhaa zinazotengenezwa nchini, pamoja na mfumo wa kusambaza taarifa za biashara nchini humo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatatu, tarehe 5 Julai 2021 na Waziri wa Viwanda na Biashara, Prof. Kitila Mkumbo, katika ufunguzi wa maonesho ya 45 ya kimataifa ya biashara ‘Sabasaba’, mkoani Dar es Salaam. Maonesho hayo yamefunguliwa na Makamu wa Rais, Dk. Phillip Mpango.

“Katika maonesho ya miaka 45, tumepanga kuzindua huduma na bidhaa mbalimbali mpya katika sekta ya viwanda, kwanza tutazindua nembo maalumu itakayotambulisha bidhaa za viungo vinavyozalishwa nchini,” amesema Prof. Mkumbo.

Prof. Mkumbo amesema, huduma hizo zitazinduliwa katika maonesho hayo na kwamba uzinduzi wa mfumo wa usambazaji taarifa za biashara, utafanywa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk. Faustine Ndugulile.

“Pili, tutazindua mfumo maalumu wa kusambaza taarifa za biashara, utakaowezesha kufahamu fursa na taratibu za kufanya biashara nchini,” amesema Prof. Mkumbo.

Pia, Prof. Mkumbo amesema, katika maonesho hayo kutafanyika uzinduzi wa duka la kidigitali.

“Tatu, tutazindua mfumo wa duka la kidigitali, utafanywa na Dk. Ndugulile katika maonesho haya,” amesema Prof. Mkumbo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!