Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Takukuru yakwama kuwahoji viongozi ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Takukuru yakwama kuwahoji viongozi ACT-Wazalendo

Ado Shaibu, Katibu Mkuu ACT-Wazalendo
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru) imeshindwa kuwahoji viongozi waandamizi wa Chama cha ACT-Wazalendo, kwa kile kilichodaiwa kuwa Ofisa aliyetakiwa kuwahoji hayupo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Viongozi wa ACT-Wazalendo ambao walitakiwa kuhojiwa ni Ado Shaibu Katibu  wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho na Dorothy Temu, Katibu Mkuu wa Chama hicho.

Leo Tarehe 25 Juni  2019,  viongozi hao waliitwa makao makuu ya Ofisi za Takukuru yaliyokuwepo Upanga jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.

Viongozi hao waliwasili kwenye Ofisi za Takukuru saa 7 na robo mchana na baadaye saa 8 kamili walielekea ghorofa ya juu kwa ajili ya kusikiliza wito wao ambapo waliambiwa kuwa Ofisa aliyewaita hayupo hivyo wataitwa siku nyingine.

Ado ameiambia MwanaHALISI ONLINE kuwa hadi wakati huu hawajaambiwa lengo la wito huo lakini kutokana na chama chao kimekuwa kikiubua mijadala mbalimbali inayohusu uchumi wa nchi inawezekana ikiwa ni moja ya sababu ya taasisi hiyo kuwaita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!