Saturday , 10 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Takukuru yakwama kuwahoji viongozi ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Takukuru yakwama kuwahoji viongozi ACT-Wazalendo

Ado Shaibu, Katibu Mkuu ACT-Wazalendo
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru) imeshindwa kuwahoji viongozi waandamizi wa Chama cha ACT-Wazalendo, kwa kile kilichodaiwa kuwa Ofisa aliyetakiwa kuwahoji hayupo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Viongozi wa ACT-Wazalendo ambao walitakiwa kuhojiwa ni Ado Shaibu Katibu  wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho na Dorothy Temu, Katibu Mkuu wa Chama hicho.

Leo Tarehe 25 Juni  2019,  viongozi hao waliitwa makao makuu ya Ofisi za Takukuru yaliyokuwepo Upanga jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.

Viongozi hao waliwasili kwenye Ofisi za Takukuru saa 7 na robo mchana na baadaye saa 8 kamili walielekea ghorofa ya juu kwa ajili ya kusikiliza wito wao ambapo waliambiwa kuwa Ofisa aliyewaita hayupo hivyo wataitwa siku nyingine.

Ado ameiambia MwanaHALISI ONLINE kuwa hadi wakati huu hawajaambiwa lengo la wito huo lakini kutokana na chama chao kimekuwa kikiubua mijadala mbalimbali inayohusu uchumi wa nchi inawezekana ikiwa ni moja ya sababu ya taasisi hiyo kuwaita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!