Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Taasisi ya urais haiwezi kuendeshwa kwa rimoti: Chongolo
Habari za Siasa

Taasisi ya urais haiwezi kuendeshwa kwa rimoti: Chongolo

Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo
Spread the love

 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema hakuna mtu anayeweza kuiendesha taasisi ya urais “kwa rimoti” na kwamba watu wanaofikiria hivyo “ni kuwa na mawazo finyu.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yameelezwa leo Ijumaa tarehe 18 Machi 2022 na Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo wakati akijibu swali la mwandishi wa habari kuhusu fununu za wastaafu wa Urais kuwa nyuma ya yanayofanywa na Serikali.

Chongolo amesema urais si mtu bali ni taasisi na ndiyo yenye mamlaka ya mwisho juu ya mambo yote yanayofanyika nchini.

“Mtu ambaye anaweza kuonekana na upofu wa kiuongozi, ni yuke anayeweza kufikiria kwamba mamlaka ya urais yanaweza kuwa controlled (kuongozwa) kwa rimoti unakaa huku anasema kata kulia, kata kushoto. Urais ni taasisi ni ngumu sana taasisi ya urais kuongozwa kwa rimoti, mamlaka hayo ni ya Rais na si mtu mwingine yeyote, mimi Katibu Mkuu wa CCM lakini siwezi kuwa na hisia hata fikra kidogo kuwa naweza kuamulia mamlaka ya rais ya kufanya ninachotaka mimi,” amesema Chongolo.

https://www.youtube.com/watch?v=41yWIFhOQtc

“Sasa huyo ambaye anamadaraka makubwa kuliko sisi ambao ndio chama tawala nandio wenye kuongoza nchi yuko wapi, aje hapa atuambie yeye anatumia njia gani ya kushawishi maslahi yake kifanywe na mamlaka.

“Msione Rais halafu mkamwangalia hivi tu, mtu anayemwangalia rais kwa wasiwasi ana tatizo nab ado hajakomaa. Mtu yeyote anayejua Rais ni mkuu wa taasisi ya urais hawezi kuchezea taasisi na mamlaka yake. Yeye akinyanyua kalamu na kuishusha chini kuna watu hawalali kuhakikisha hayo mambo yanatokea,” amesema.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!