Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sophia Simba ajitosa uspika, wafikia 17
Habari za Siasa

Sophia Simba ajitosa uspika, wafikia 17

Spread the love

 

ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania, Sophia Simba amekuwa miongoni mwa. Wanachama 17 wa chama hicho, kuchukua fomu ya kuwania uspika wa Bunge wan chi hiyo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Sophia aliyewahi kuhudumu wizara mbalimbali katika utawala wa awamu ya nne wa Jakaya Kikwete, amechukua fomu leo Jumanne, tarehe 11 Januari 2022, ofisi ndogo za CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.

Mchakato wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kuwania nafasi hiyo iliyoachwa wazi na Job Ndugai aliyejizulu, imeanza jana Jumatatu 10 hadi 15 Januari 2022.

Akizungumza Makao Makuu ya CCM jijini Dodoma, Solomon Itunda Katibu msaidizi mkuu idara ya oganizesheni amesema leo Jumanne Ofisi kuu ya CCM, Dodoma waliochukua fomu ni watatu na Ofisi ndogo ya Lumumba Dar es Saalam ni watano na kufikisha jumla ya wanachama 17 yangu mchakato uanze jana Jumatatu.

Kati ya waliochukua fomu ya kugombea nafasi ya Uspika ni pamoja na mwanasiasa mkongwe ndani ya siasa za CCM na ambaye amewahi kuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake CCM (UWT) pamoja na kushika wadhifa mbalimbali Sophia Simba.

Itunda amewataja waliochukua fomu ya kugombania nafasi ya usipika katika ofisi ndogo ya Lumumba Jijini Dar es salaam kuwa ni Joseph Msukuma, Goodluck Ole-Madeve, Sophia Simba.

Amewataja wengine kuwa ni pamoja na Juma Chum,Baraka Byabato,Musaa Zungu Emmanuel Mwakasaka na Prof. Handley Mafwenga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!