Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Michezo Singida Big Stars yamwita Rais Samia
Michezo

Singida Big Stars yamwita Rais Samia

Spread the love

TIMU ya Singida Fountain Gate, maarufu kama Singida Big Stars, imemwalika Rais Samia Suluhu ahudhurie katika mechi zake  kama anavyofanya kwa timu nyingine kubwa nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida…(endelea).

Mwaliko huo umetolewa jana na Singida Big Stars, wakati wanazungumzia ujio wa Rais Samia mkoani Singida, ambaye anafanya ziara ya kikazi ya siku mbili inayoishia leo tarehe 16 Oktoba 2023.

Mbali na kumuomba Rais Samia ahudhurie katika mechi zake, Msemaji wa Singida Big Stars, Hussein Masanza amesema wanajipanga kushiriki michuano ya kimataifa ili wanufaike na ofa yake ya kupata milioni tano kwa kila goli, aliyoahidi kutoa kwa timu za Tanzania zitakazoshiriki katika michuano hiyo.

“Nilitamani ifike siku ya leo tupate fursa ya kumwalika katika mechiz zetu, tuna mechi nyingi tunazesha tungefurahi kumualika hata Dodoma akipata nafasi aje. Tumezoea kumuona mama yetu akienda mechi za Simba na Yanga, siku moja aje za Singida,” amesema Masanza na kuongeza:

“Tunafahamu mama ni mwanamichezo, hamasa zake tumeziona tungetamani kuwa miongoni mwa wanufaika wa goli la mama sababu tumeshiriki michuano ya kimataifa bahati mbaya tumetolewa Misri, lakini tunajipanga msimu ujao tupate goli la mama.”

Kwa upande wake mchezaji wa timu hiyo, Habib Kyombo, amesema “tumeguswa sana kwa kujitoa kwake michezo yetu na michezo ameweka goli la mama kila timu zinazoshiriki mashindano makubwa , na sisi tunajiandaa vizuri ili msimu ujao tuweze kupata goli la mama.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Pesa ipo huku Meridianbet, beti sasa

Spread the love  WIKIENDI inaishia leo hii jaman kama bado hujasuka mkeka...

Michezo

Wenzako wameshakuwa mamilionea hapa wewe unasubiri nini?

Spread the love  WIKIENDI imefika na ukiachana na mvua za Dar es...

Michezo

Manchester City vichwa chini Ligi Kuu England

Spread the love MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Uingereza klabu yaManchester City...

Michezo

Piga mkwanja wa kutosha katika usiku wa kibabe kati ya Man United vs Chelsea

Spread the love USIKU wa leo katika dimba la Old Trafford utapigwa mchezowa...

error: Content is protected !!