MAHAKAMA Kuu ya Tanzania imesogeza mbele kwa siku moja (sawa na saa 24) sherehe za Siku ya Sheria kutoka tarehe 1 Februari hadi 2 Februari 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Taarifa iliyotolewa jana Jumamosi, tarehe 29 Januari 2022 na Tiganga Vincent, Mkuu wa Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano wa Mahakama ilieleza, sababu zisizozuilikwa.
Vicent alisema, sherehe hizo zitaanza saa 2:00 asubuhi katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma na mgeni rasmi atakuwa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
“Uongozi wa Mahakama unaomba radhi kwa usumbufu wowote kufuatia mabadiliko haya,” alisema Vicent
Leave a comment