Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Sh66.86 Bil. zakusanywa tozo daraja la Kigamboni
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sh66.86 Bil. zakusanywa tozo daraja la Kigamboni

Spread the love

 

SERIKALI imesema jumla ya Sh66.86 bilioni zimekusanywa tangu kuanza kutoza tozo za kuvuka daraja la Kigamboni mwaka 2016. Anaripti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yameelezwa leo Ijumaa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, akijibu swali la Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndungulile aliyetaka kujua kiasi kilichokusanywa hadi sasa katika daraja hilo.
Pia Ndungulile alitaka kujua mpango wa Serikali kufanya huduma za daraja hilo kuwa bure.

Akijibu swali hilo Kasekenya amesema kuwa Mfuko wa NSSF ulianza kupokea fedha zitokanazo na tozo kwa watumiaji wa Daraja la Nyerere mnamo tarehe 14 Mei, 2016 baada ya kuzinduliwa.

“Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Mei, 2022, Mfuko ulikuwa umekusanya jumla ya Shilingi Bilioni 66.86,” amesema.
Aidha amesema Serikali imeendelea kupunguza tozo kwa watumiaji wa Daraja hilo tangu kuzinduliwa kwake kwa kuzingatia tathmini ya uwezo wa wananchi kumudu tozo hizo.

“Kwa mara ya mwisho, Serikali imepunguza tozo husika tarehe 21 Mei, 2022,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!